Kamati ya Fedha na utawala imekagua miradi inayoendelea kutekelezwa ikiwa ni utaratibu wa kukagua miradi kipindi cha robo ya pili kwa mwaka wa fedha 2025/2026, Katika Ziara hiyo Kamati ya Fedha wamepongeza Timu ya Menejimenti kwa usimamiaji mzuri wa Miradi na kutoa maelekezo kuwa ifikapo Februari 20 miradi yote iwe imekamilika kwa 100%.
Ziara hiyo imefanyika Februari 4, 2026 katika maeneo mbalimbali ikiwemo Ujenzi wa shule mpya ya awali na msingi Joel Bendera, ujenzi wa madarasa 2 ya mfano ya Awali, madarasa 3 ya msingi na matundu 12 ya vyoo katika kituo shikizi cha Kitifu,Ujenzi wa madarasa 3 na matundu 6 ya vyoo shule ya msingi Mbeza,Ukamilishaji wa Mnada Kwamsisi, ukamilishaji wa nyumba ya Mganga Zahanati ya Lwengera Darajani pamoja na Ujenzi wa madarasa 2 ya awali ya mfano na madarasa 3 ya msingi pamoja na matundu 6 ya vyoo katika shule shikizi ya Lwengera Relini.
Mwenyekiti wa Halmashauri Mh. Ali Mkwavingwa ambaye pia ni Mwenyekiti wa kamati ya fedha na utawala katika kikao cha majumuisho, ameishukuru serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kuleta tabasamu kwa wanafunzi na wananchi kwa kuwajengea madarasa kwani elimu ndio nguzo ya maendeleo ya kila mwanadamu. Pia kuongezeka kwa madarasa na shule kutasaidia kupunguza msongamano darasani, kutokutembea umbali mrefu kufuata shule kutasaidia kusoma katika mazingira rafiki na hatimae kuongeza ari ya kupenda elimu.
Naye Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Korogwe Bi. Zahara Msangi ameahidi miradi hiyo kukamilika kwa wakati kama kamati ilivyoelekeza.
Korogwe Tanga Tanzania
S.L.P: 615 Korogwe
Simu: 0272650050
Simu ya Kiganjani:
Barua Pepe: info@korogwetc.go.tz
Copyright©2018 Korogwe Town Council. All rights reserved.