Mkuu wa Wilaya ya Korogwe azindua Kambi ya Matibabu ya Macho
Mkuu wa Wilaya ya Korogwe Mhe. Jokate Mwegelo amezindua Kambi ya Matibabu ya Macho katika Hospitali ya Mji wa Korogwe (Magunga). Kambi hiyo ya Matibabu ya Macho ilizinduliwa Juni 02, Mwaka huu. Pamoja na uzinduzi wa Kambi hiyo, Kambi tayari ilishaanza kutoa huduma kuanzia Juni 01 na itaendelea hadi Juni 04 Mwaka huu bila ya gharama yoyote (Bure). Huduma zote za Matibabu ya Macho zinaratibiwa na Taasisi ya Al Ataa Charitable Foundation kwa udhamini wa Taasisi ya Qatar Charity.
“ Tuzingatie ushauri tutakaopewa na Wataalamu wa Macho ili tuweze kuiamarisha Macho yetu” alisema Mhe. Jokate Mwegelo ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Korogwe wakati wa uzinduzi wa Kambi ya Matibabu ya Macho. Mhe. Jokate alisisitiza kuwa pamoja na Wananchi kupatiwa Matibabu ya Macho, ni vyema kuwa na utamaduni wa kupima afya mara kwa mara ili kujua hali zao na kuweza kulijenga Taifa bila hofu yoyote.
“Tunatoa shukrani kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutupa ruhusa ya kuendelea kutao huduma za Matibabu kwa Watanzania katika kipindi chake cha uongozi” alisema Bw. Abubakar Mwinyimbegu ambaye ni Meneja Uhusiano wa Umma kutoka Taasisi ya Al Ataa Charitable Foundation. Bw. Abubakar alifafanua kuwa Taasisi hiyo itaendelea kushikamana na Watanzania katika kutoa huduma za Matibabu.
Katika hatua nyengine, Bw. Vendavenda Sumuni ambaye ni Katibu wa Afya Katika Halmashauri ya Mji wa Korogwe alisema “ Huduma zote ni bure ni vyema Wananchi wakajitokeza kwa wingi katika kuchangamkia fursa ya matibabu”. Nao Wananchi waliojitokeza kupatiwa huduma ya Matibabu ya Macho walitoa Shukrani kwa Taasisi inayoratibu Matibabu na Serikali kwa ujumla kwa kuapatiwa huduma bila gharama yoyote (Bure).
Korogwe Tanga Tanzania
S.L.P: 615 Korogwe
Simu: 0272650050
Simu ya Kiganjani:
Barua Pepe: info@korogwetc.go.tz
Copyright©2018 Korogwe Town Council. All rights reserved.