Mkuu wa Wilaya ya Korogwe azindua Shule mpya
Afisa Tarafa, Tarafa ya Korogwe Bi. Grory Sanga kwaniaba ya Mkuu wa Wilaya ya Korogwe Mhe. William Mwakilema amezindua Shule Mpya ya Sekondari ya Msambiazi iliyopo Kata ya Mtonga. Uzinduzi wa shule hiyo nihatua mojawapo ya utekelezaji wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi (CCM) kwa Vitendo pamoja na ahadi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika uboreshaji wa Miundombinu ya Elimu hapa Nchini. Uzinduzi wa Shule ya Sekondari Msambiazi umefanyika Januari 16, Mwaka huu katika viwanja vya shule hiyo katika eneo la Msambiazi.
Mradi wa Ujenzi wa Shule ya Sekondari Msambiazi umetekelezwa kwa gharama ya Shilingi Milioni Mia Tano na Themanini na Nne, fedha zote zilitolewa na Serikali Kuu kupita Mradi wa SEQUIP. Mradi wa Ujenzi wa Shule ya Sekondari Msambiazi tayari umeshakamiliaka kwa Asilimia Mia Moja ukihusisha Vyumba Nane vya Madarasa, Chumba cha Komputa, Maktaba, Maabara Tatu, Kichomea Taka pamoja na Jengo la Utawala.
“Nitoe pongezi kwa Mkurugenzi na Wataalamu wote wa Halmashashauri ya Mji wa Korogwe kwa kukamilisha Mradi huu wa shule kwa wakati” alisema Bi. Grory Sanga ambaye ni Afisa Tarafa, Tarafa ya Korogwe aliyemuwakilisha Mkuu wa Wilaya ya Korogwe Mhe. William Mwakilema katika uzinduzi wa Shule hiyo. Bi. Grory alisisitiza kuwa ni vyema Walimu na Wanafunzi wakajitahidi kutunza Mradi huo ili uweze kudumu kwaaajili ya vizazi vijavyo.
“Nitoe shukrani zangu za dhati kwa Wananchi wa Msambiazi, Kwamasimba pamoja na Antakae wa kujitoa kwa dhati katika msaragambo mpaka ufanikishaji wa shule hii, kukamilika kwa shule hii nifahari yetu wote” alisema Mhe. Francis Komba ambaye ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji wa Korogwe. Nao Wananchi wa Mtaa wa Msambiazi ambao ni wanufaika wa Mradi wa Ujenzi wa Shule ya Sekondari Msambiazi walitoa shukrani zao kwa Serikali kwa utekelezaji wa Shule hiyo jirani na maeneo yao.
Korogwe Tanga Tanzania
S.L.P: 615 Korogwe
Simu: 0272650050
Simu ya Kiganjani:
Barua Pepe: info@korogwetc.go.tz
Copyright©2018 Korogwe Town Council. All rights reserved.