Waratibu wa Mwenge wa Uhuru watembelea Miradi ya Mendeleo Mji wa Korogwe
Timu ya Uratibu wa Mwenge wa Uhuru Mkoa wa Tanga ikiambatana pamoja na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Korogwe pamoja na Wataalamu mbalimbali wa Taasisi za Serikali zilizopo Mji wa Korogwe imetembelea Miradi ya Maendeleo iliyopendekezwa kupitiwa na Mwenge wa Uhuru Mwaka huu. Mwenge wa Uhuru kwa Mwaka 2024, unatarajiwa kuwasili katika Mji wa Korogwe Aprili 10, Mwaka huu. Ziara hiyo ya Timu ya Waratibu wa Mbio za Mwenge ilifanyika Februari 26, Mwaka huu katika maeneo mbalimbali ya Mji wa Korogwe.
Kauli Mbiu ya Mwenge wa Uhuru kwa Mwaka 2024 ni: “Tunza Mazingira na Shiriki Uchaguzi wa Serikali za Mitaa kwa Maendeleo Endelevu”
Timu ya Uratibu wa Mwenge ilitembelea Miradi mbalimbali ya Maendeleo iliyopendekezwa kupitiwa na Mwenge wa Uhuru Mwaka 2024 ili Timu ya Uratibu wa Mwenge iweze kujiridhisha kukamilika kwa Miradi hiyo. Miradi hiyo ni pamoja na Mradi wa Tanki la Maji katika Eneo la Bagamoyo, Ujenzi wa Nyumba ya Mwalimu Shule ya Sekondari New Bagamoyo, Kikundi cha Vijana cha Kisimo kinachojishughulisha na Ujenzi, Uchoraji wa Ramani za Majengo pamoja na Utengenezaji wa Mapambo.
Miradi Mingine ya Maendeleo ni Ukamilishaji wa Zahanati ya Lwengera Darajani, Matengenezo ya Barabara ya White House Kilomita 0.57 kwa Kiwango cha Lami, Shughuli za Uhifadhi wa Mazingira zinazofanywa na Forest Focus, Shughuli za Uchaguzi wa Serikali za Mitaa Shule ya Msingi Kilimani, Pamoja na Shughuli za Kikundi cha Watu wenye uhitaji Maalumu Shule ya Msingi Kilimani katika Kitengo cha Watu Wenye Uhitaji Maalumu.
“Natoa pongezi kwa maandalizai mazuri ya Miradi ya Maendeleo, natumaini baadhi ya changamoto ndogondogo zilizojitokeza katika miradi zitakamilishwa ndani ya muda mfupi” Alisema Bw. Timotheo Sosia amabye ni Mratibu wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Mkoa wa Tanga Mwaka 2024 wakati wa ziara ya kukagua Miradi ya Maendele iliyopendekezwa kupitiwa na Mwenge wa Uhuru katika Mji wa Korogwe. Bw. Sosia alisisitiza kuwa Miradi yote iliyopendekezwa itaendelea kufanyiwa ukaguziwa mpaka zoezi la Mbio za Mwenge litakapokamilika.
Korogwe Tanga Tanzania
S.L.P: 615 Korogwe
Simu: 0272650050
Simu ya Kiganjani:
Barua Pepe: info@korogwetc.go.tz
Copyright©2018 Korogwe Town Council. All rights reserved.