• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Mji wa Korogwe
Halmashauri ya Mji wa Korogwe

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Korogwe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Afya
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi waJamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Mazingira na Udhibiti Taka Ngumu
    • Vitengo
      • Tehama na Uhusiano
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
    • Mifugo
    • Kilimo
  • Huduma Zetu
    • Za afya
    • Kielimu
    • Za Maji
    • Za kilimo
    • Mifugo
    • Huduma za watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Elimu, afya,uchumi na maji
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Picha za Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

Benki ya TADB yatoa mkopo kwa wafugaji wa Mji wa Korogwe

Posted on: February 5th, 2021

Benki ya TADB  yatoa mkopo kwa wafugaji wa Mji wa Korogwe

Chama cha Ushirika cha Wafugaji wa ng’ombe wa maziwa Mjini Korogwe (UWAKO) kimepata mkopo wa ng’ombe thelathini wa maziwa kutoka Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB). Mkopo huo wa ng’ombe thelathini una thamani ya Shilingi Milioni Sitini na mkopo utalipwa kwa muda wa Miaka Mitatu. Wanachama waliokithi vigezo wamekabidhiwa ng’ombe hao Februari 5, mwaka huu katika ofisi za chama cha UWAKO ziliyopo eneo la Majengo.

“Vijana tunatakiwa kuchangamkia fursa za ufugaji ili kujikomboa kiuchumi” alisema Bi. Farida Ponda ambaye ni Mwenyekiti wa Chama cha ushirika cha ufugaji wa ng'ombe wa maziwa Mji wa Korogwe  (UWAKO). Bi. Farida alifafanua kuwa Lengo kuu la Benki ya maendeleo ya kilimo Tanzania (TADB)   kutoa  mkopo wa  go’ombe wa maziwa kwa  wafugaji hao ni kuimarisha kipato cha wafugaji na sekta ya mifugo kwa ujumla hapa nchini katika harakati za kuelekea uchumi wa viwanda.

“ Wafugaji mjiepushe kuwatumia  madaktari vishoka (madakatari wa mtaani) kutibu ng’ombe zenu” alisema  Dr. Fortunatas Silayo ambaye ni Afisa Mifugo kutoka Halmadhauri ya Mji wa Korogwe wakati akikabidhi ng’ombe hao kwa wanachama wa UWAKO.  Dr. Silayo alisisitiza zaidi kwa kusema “ili mfugaji upate  maziwa ya kutosha ni vyema kuwapa ngombe malisho bora pamoja na kufuata ushauri unaotolewa na  wataalamu wa mifugo”.

Kwa upande mwingine Ndugu Denisi Nguruse ambaye ni Afisa Ushirika wa Halmashauri ya Mji wa Korogwe alitoa nasaha kwa wanufaika wa mkopo wa ng’ombe kwa kusema “mhakikishe ng’ombe mliopewa mnawaweka kwenye mabanda bora”. Nae Bi. Yusta Luoga ambaye ni mnufaika wa mkopo wa ng’ombe wa maziwa aliishukuru Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) na Ushirika wa UWAKO kwa ujumla kwa kufungua fursa za kiuchumi kwa vijana wa Mji wa Korogwe.

Matangazo

  • Tangazo la Kazi - Afya December 06, 2024
  • TANGAZO LA KAZI - AFYA November 26, 2024
  • ERMS OF REFERENCE FOR THE PROVISION OF CONSTRUCTION SUPERVISION CONSULTANCY SERVICES FOR URBAN INFRASTRUCTURE DEVELOPMENT IN KOROGWE TOWN UNDER THE TACTIC PROJECT March 09, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • Waratibu Elimu kata na Wali Wakuu wa Shule za Msingi za Mji wa Korogwe wajengewa uwezo wa usimamizi wa ufundishaji na Ujifunzaji.

    June 27, 2025
  • Mradi wa TACTIC kuimarisha Huduma za Usafirishaji kwa Miji 12 Tanzania.

    June 26, 2025
  • Halmashauri ya Mji wa Korogwe yaadhimisha Siku ya Wajane Duniani.

    June 23, 2025
  • Shule ya Msingi Kwamngumi yalima Hekari mbili za Mahindi

    June 19, 2025
  • Angalia Zote

Video

Video Zaidi

Kurasa Muhimu

  • Ukodishaji wa Ukumbi
  • Ukasanyaji wa Taka

Tovuti Zinazohusiana

  • TOVUTI YA SERIKALI
  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • MKOA TANGA
  • TUME YA AJIRA
  • PPRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Korogwe Tanga Tanzania

    S.L.P: 615 Korogwe

    Simu: 0272650050

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@korogwetc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright©2018 Korogwe Town Council. All rights reserved.