• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Mji wa Korogwe
Halmashauri ya Mji wa Korogwe

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Korogwe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Afya
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi waJamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Mazingira na Udhibiti Taka Ngumu
    • Vitengo
      • Tehama na Uhusiano
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
    • Mifugo
    • Kilimo
  • Huduma Zetu
    • Za afya
    • Kielimu
    • Za Maji
    • Za kilimo
    • Mifugo
    • Huduma za watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Elimu, afya,uchumi na maji
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Picha za Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

DC ahimiza madiwani kushirikiana na watumishi kuondoa kero za wananchi

Posted on: February 8th, 2019

Mkuu wa wilaya ya Korogwe Bi. Kissa Kasongwa amewataka madiwani wa Halmashauri ya mji wa Korogwe kuendelea kushirikiana na watumishi kuanzia ngazi ya serekali za mitaa hadi mkurugenzi ili waweze kutatua changamoto za wananchi kama vile elimu, afya , maji na miundombinu.

Akizungumza  katika kikao cha madiwani cha robo ya pili ya mwaka kilichofanyika jana katika ukumbi wa halmashauri ya mji wa Korogwe alisema  “madiwani wanapaswa kufanya kazi na watumishi waliopo katika kata zao kwa pamoja” akitoa mfano wa ugawaji wa vitambulisho vya wajasiriamali wadogo ambapo alianisha kuwa halmashauri ya mji iliweza kumaliza vitambulisho 1500 walivyopangiwa na Mkoa na kuwataka waendelee kushirikiana kugawa vingine walivyopewa tena.Pia aliagiza ujenzi wa  kituo cha afya cha majengo,  vyumba vya madarasa na miundombinu mingine ya shule za sekondari na msingi vikamilike  muda uliokusudiwa ili changamoto za afya na elimu zipungue.

Naye katibu tawala wa Wilaya ya Korogwe Bi.Rehema Mbwasi alisema kuwa taratibu za kukabidhiana hospitali ya Magunga ambayo kwa sasa inaendeshwa na halmashauri ya Wilaya ya Korogwe vijijini zimekamilika ila anasubiriwa Mhe. Mbunge ambaye yupo kwenye vikao vya bunge ili wafanye mkutano wa pamoja kati ya halmashauri ya mji na vijijini.Pia alisema mchakato wa maombi ya wanakijiji wa Kwemasimba kutaka kujumuishwa katika eneo la halmashauri ya mji badala ya halmashauri ya Korogwe vijijini umeshafikia pazuri baada ya kamati iliyoundwa kwa ajili ya suala hilo kuwazilisha taarifa yake.

Aidha mwenyekiti wa halmashauri Mhe. Hilary Ngonyani kabla ya kuruhusu maamuzi na mapendekezo ya kamati mbalimbali za madiwani kuwasilishwa; alisema kuwa tayari alishaongea na Mkurugenzi wa maji Tanga na kumhakikishia kwamba kuhusu suala la usambazaji wa maji katika mji wa Korogwe tayari lipo katika hatua ya zabuni.Pia akipokea taarifa ya mapato na matumizi kutoka kamati ya fedha na utawala ilionekana kuwa Halmashauri imekusanya kiasi cha Tsh 78,942,456 kutoka mapato ya ndani na imepokea ruzuku ya Tsh 1,306,396,350 toka serekali kuu na kufanya jumja ya mapato kwa mwezi Decemba, 2018 kuwa 1,385,339,106 na hivyo mapato kuanzia july 2018 hadi Decemba 2018 kuwa 8,560,103,545.65 sawa na asilimia 35.28 ya makisio ya Tsh 24,261,132,948.

Matangazo

  • Tangazo la Kazi - Afya December 06, 2024
  • TANGAZO LA KAZI - AFYA November 26, 2024
  • ERMS OF REFERENCE FOR THE PROVISION OF CONSTRUCTION SUPERVISION CONSULTANCY SERVICES FOR URBAN INFRASTRUCTURE DEVELOPMENT IN KOROGWE TOWN UNDER THE TACTIC PROJECT March 09, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • Waratibu Elimu kata na Wali Wakuu wa Shule za Msingi za Mji wa Korogwe wajengewa uwezo wa usimamizi wa ufundishaji na Ujifunzaji.

    June 27, 2025
  • Mradi wa TACTIC kuimarisha Huduma za Usafirishaji kwa Miji 12 Tanzania.

    June 26, 2025
  • Halmashauri ya Mji wa Korogwe yaadhimisha Siku ya Wajane Duniani.

    June 23, 2025
  • Shule ya Msingi Kwamngumi yalima Hekari mbili za Mahindi

    June 19, 2025
  • Angalia Zote

Video

Video Zaidi

Kurasa Muhimu

  • Ukodishaji wa Ukumbi
  • Ukasanyaji wa Taka

Tovuti Zinazohusiana

  • TOVUTI YA SERIKALI
  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • MKOA TANGA
  • TUME YA AJIRA
  • PPRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Korogwe Tanga Tanzania

    S.L.P: 615 Korogwe

    Simu: 0272650050

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@korogwetc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright©2018 Korogwe Town Council. All rights reserved.