• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Mji wa Korogwe
Halmashauri ya Mji wa Korogwe

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Korogwe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Afya
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi waJamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Mazingira na Udhibiti Taka Ngumu
    • Vitengo
      • Tehama na Uhusiano
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
    • Mifugo
    • Kilimo
  • Huduma Zetu
    • Za afya
    • Kielimu
    • Za Maji
    • Za kilimo
    • Mifugo
    • Huduma za watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Elimu, afya,uchumi na maji
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Picha za Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

Hospitali ya KCMC yatoa matibabu ya macho Mji wa Korogwe

Posted on: June 16th, 2021

Hospitali ya KCMC yatoa matibabu ya macho Mji wa Korogwe 

Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Kaskazini ya KCMC iliyopo Moshi Mkoani Kilimanjaro kwa kushirikiana na Halmashauri ya Mji wa Korogwe imetoa matibabu ya macho kwa Wananchi wa Mji wa Korogwe na Maeneo ya jirani. Matibabu hayo ya Macho yalijumuisha uchunguzi wa macho kwa ujumla, upasuaji wa mtoto wa jicho, utoaji wa miwani pamoja na utoaji wa dawa za macho. Matibabu yalitolewa  kuanzia Juni 14 na yataendelea hadi Juni 17 mwaka huu katika Kituo cha Afya cha Majengo kilichopo Kata ya Majengo.

“Hospitali ya Rufaa ya KCMC tumejipanga vyema kuhakikisha tunatatua  matatizo ya  macho kwa Wananchi wa Mji wa Korogwe na Kanda ya Kaskazini kwa ujumla” alisema Dr. Alex Lissu ambaye ni Mratibu wa  Huduma za Macho ya Kliniki Tembezi katika Hospitali ya Rufaa ya KCMC. Dr Lissu alitoa nasaha kwa kusema “mtoto wa jicho na matatizo ya macho kwa ujumla yanatibika hivyo wanachi wa Mji wa Korogwe wajitokeze kwa wingi ili tuwapatie matibabu”.

Kwa upande mwengine, Dr. Alex Lissu alifafanua kuwa kwa siku Nne mfululizo waliopo Kituo cha Afya cha Majengo walipanga kuwafanyia uchunguzi wa macho watu Mia Nne na kuwafanyia upasuaji wa macho watu Mia Moja. Pia alifafanua zaidi kuwa Wananchi wengi waliofanyiwa uchunguzi wa macho walibainika kuwa na matatizo ya macho ikiwa ni pamoja na mtoto wa jicho, matatizo ya macho kwa watu wazima, na presha ya macho. Matatizo mengine ni ukungu wa macho, upungufu wa kuona, pamoja na shida ya macho inayosababiswa na sukari.

“Tunatoa shukrani kwa Hospitali ya Rufaa ya KCMC kwa kuwapatia matibabu ya macho Wananchi wa Mji wa Korogwe” alisema Dr. Theresia Mauya ambaye ni Mganga Mfawidhi wa Kituo cha Afya cha Majengo. Dr. Mauya alifafanua kuwa ushirikiano kati ya Hospitali ya Rufaa ya KCMC na Halmashauri ya Mji wa Korogwe katika matibabu ya macho ni wa kindugu na  utakuwa ni endelevu katika kutatua changamoto ya macho kwa Wananchi wa Mji wa Korogwe.

Nae Ndugu. Lucas Zimamoto ambaye ni Mratibu wa Matibabu ya Macho katika Halmashauri ya  Mji wa Korogwe alisema “ muitikio wa  Wananchi waliojitokeza kupatiwa matibabu ya macho kwa gharama nafuu ni mzuri”. Kwa upande mwengine, Mzee Fadhili Chiliavyangu ambaye ni Mwananchi wa Mji wa Korogwe aliyejitokeza kupatiwa matibabu alisema “tunatoa shukrani kwa Wataalamu wote kutoka Hospitali ya Rufaa ya KCMC  pamoja na  Wataalamu  wa Kituo cha Afya cha Majengo kwa kutupatia matibabu ya macho kwa gharama nafuu”.

Matangazo

  • Tangazo la Kazi - Afya December 06, 2024
  • TANGAZO LA KAZI - AFYA November 26, 2024
  • ERMS OF REFERENCE FOR THE PROVISION OF CONSTRUCTION SUPERVISION CONSULTANCY SERVICES FOR URBAN INFRASTRUCTURE DEVELOPMENT IN KOROGWE TOWN UNDER THE TACTIC PROJECT March 09, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • Waratibu Elimu kata na Wali Wakuu wa Shule za Msingi za Mji wa Korogwe wajengewa uwezo wa usimamizi wa ufundishaji na Ujifunzaji.

    June 27, 2025
  • Mradi wa TACTIC kuimarisha Huduma za Usafirishaji kwa Miji 12 Tanzania.

    June 26, 2025
  • Halmashauri ya Mji wa Korogwe yaadhimisha Siku ya Wajane Duniani.

    June 23, 2025
  • Shule ya Msingi Kwamngumi yalima Hekari mbili za Mahindi

    June 19, 2025
  • Angalia Zote

Video

Video Zaidi

Kurasa Muhimu

  • Ukodishaji wa Ukumbi
  • Ukasanyaji wa Taka

Tovuti Zinazohusiana

  • TOVUTI YA SERIKALI
  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • MKOA TANGA
  • TUME YA AJIRA
  • PPRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Korogwe Tanga Tanzania

    S.L.P: 615 Korogwe

    Simu: 0272650050

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@korogwetc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright©2018 Korogwe Town Council. All rights reserved.