• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Mji wa Korogwe
Halmashauri ya Mji wa Korogwe

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Korogwe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Afya
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi waJamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Mazingira na Udhibiti Taka Ngumu
    • Vitengo
      • Tehama na Uhusiano
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
    • Mifugo
    • Kilimo
  • Huduma Zetu
    • Za afya
    • Kielimu
    • Za Maji
    • Za kilimo
    • Mifugo
    • Huduma za watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Elimu, afya,uchumi na maji
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Picha za Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

Komba: Madiwani ongezeni nguvu katika usimamizi wa Miradi ya Maendeleo

Posted on: April 25th, 2023

Komba: Madiwani ongezeni nguvu katika usimamizi wa Miradi ya Maendeleo

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji wa Korogwe Mhe. Francis Komba amewataka Madiwani wa Halmashauri hiyo kuongeza nguvu katika usimamizi wa Miradi ya Maendeleo ili iweze kukamilika kwa wakati kwa lengo la kuwahudumia Wananchi. Kauli hiyo aliitoa Aprili 25, Mwaka huu wakati Kamati ya Fedha na Utawala ilipotembelea Miradi ya Maendeleo katika Maeneo mbalimbali ya Mji wa Korogwe.

“Waheshimiwa Madiwani ongezeni nguvu katika usimamizi wa Miradi ya maendeleo ili iweze kukamilika kwa wakati” alisema Mhe. Francis Komba wakati wa ziara ya kutembelea Miradi ya Maendeleo katika Mji wa Korogwe. Mhe. Komba alifafanua kuwa swala la usimamizi wa Miradi sio jukumu la Mkurugenzi na Wataalamu wa Halmashauri pekeyeo, hivyo ni vyema Madiwani wakaongeza nguvu ili kuharakisha kukamilika kwa miradi hiyo.

Katika hatua nyengine, Mhe. Komba amemshauri Mkurugenzi  wa Halmashuri ya Mji wa Korogwe kuendeleza utamaduni wa uwazi katika utoaji Kandarasi za Ujezi pamoja na ushirikishwaji wa Kamati za Ujezi katika  Manunuzi ya Vifaa ili kuleta umoja na mshikamano katika usimamizi wa Miradi. Mhe Komba alisema “Tuendeleze utawaduni wa uwazi katika utoaji wa Kandarasi za Ujezi pamoja na Manunuzi ya Vifaa ili kuondoa ukakasi kwa Wananchi”

“Mheshiwa Mwenyekiti, Madiwani tuko tayari katika kuongeza nguvu katika usimamizi wa Miradi ili iweze kukamilika kwa haraka”alisema Mhe. Nassoro Mohamed amabye ni Diwani wa Kata ya Kwamsisi. Mhe. Nassoro alifafanua kuwa Miradi ya Maendeleo inapokamilika kwa wakati ni jambo jema kwa Mkurugenzi pamoja na Madiwani kwa ujumla. Nae Bw. Elinlaa Kivaya ambaye ni Mchumi wa Halmashauri ya Mji wa Korogwe anayemwakilisha Mkurugenzi alisema “Mwenyekiti maelekezo yote uliyotupa tumeyapokea na tutatekeleza”.

Ziara ya Kamati ya Fedha na Utawala inayojumuisha Madiwani pamoja na Wataalamu wa Halmashauri ilitembelea Miradi mbalimbali katika kuhitimisha Robo ya Tatu katika Mwaka wa Fedha 2022/23. Miradi ya Maendeleo iliyotembelewa ni Pamoja na Mradi wa Ujenzi wa Vibanda vya Biashara katika Uwanja wa Manundu, Ujenzi wa Barabara ya Lami Hojana / Magufuli (Mt.View),  pamoja na Ujenzi wa Zahanati ya Old Korogwe ( Lwengera Darajani).

Miradi mingine ni pamoja na Ujenzi wa Zahanati ya Kilole ( Kilole Manzese), Ujenzi wa Mifereji katika Barabara ya Madaraka (Kilole Darajani), Ujenzi wa Bweni la Watoto wenye Mahitaji Maalumu katika Shule ya Msingi Kwamngumi, pamoja na Ujenzi wa Kituo cha Pamoja cha Kibiashara kilichopo Makao Makuu ya Halmashauri.

Matangazo

  • MAJINA YA WATU WALIOITWA KWENYE USAILI - KOROGWE TC July 05, 2022
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI May 24, 2022
  • KOROGWE GIRLS S.S JOINING INSTRUCTIONS 2020/2021 December 15, 2020
  • KWAMNDOLWA S.S JOINING INSTRUCTIONS 2020/2021 December 15, 2020
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • Shule ya Sekondari Semkiwa yapata Msaada wa Kompyuta

    August 23, 2023
  • Mwanaidi Rajabu: Acheni kutumia muda wa kazi za Umma kufanya kazi binafsi

    August 22, 2023
  • Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji wa Korogwe atembelea Miradi ya Maendeleo

    August 18, 2023
  • Mkurugenzi wa Mji wa Korogwe apokea Cheti cha Shukrani kutoka Shirika la US Peace Corps Tanzania

    July 12, 2023
  • Angalia Zote

Video

Video Zaidi

Kurasa Muhimu

  • Ukodishaji wa Ukumbi
  • Ukasanyaji wa Taka

Tovuti Zinazohusiana

  • TOVUTI YA SERIKALI
  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • MKOA TANGA
  • TUME YA AJIRA
  • PPRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Korogwe Tanga Tanzania

    S.L.P: 615 Korogwe

    Simu: 0272650050

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@korogwetc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright©2018 Korogwe Town Council. All rights reserved.