• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Mji wa Korogwe
Halmashauri ya Mji wa Korogwe

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Korogwe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Afya
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi waJamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Mazingira na Udhibiti Taka Ngumu
    • Vitengo
      • Tehama na Uhusiano
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
    • Mifugo
    • Kilimo
  • Huduma Zetu
    • Za afya
    • Kielimu
    • Za Maji
    • Za kilimo
    • Mifugo
    • Huduma za watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Elimu, afya,uchumi na maji
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Picha za Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

Komba: Madiwani pamoja na Wataalamu twendeni kwa Wananchi tukahamasishe Sensa

Posted on: July 28th, 2022

Komba: Madiwani pamoja na Wataalamu twendeni kwa Wananchi tukahamasishe Sensa

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji wa Korogwe Mhe. Francis Komba amewataka Madiwani pamoja na Wataalamu wa Halmashauri ya Mji wa Korogwe kuunga mkono jitihada za Serikali katika ushiriki pamoja uhamasishaji wa zoezi la Sensa linalotatarajiwa kufanyika Agosti 23, Mwaka huu. Agizo hilo alilitoa wakati wa Baraza la Madiwani la Kawaida la Robo ya Nne linalohitimisha Mwaka wa Fedha 2021/22 lililofanyika Julai 28, Mwaka huu katika ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri ya Mji wa Korogwe.

“Madiwani pamoja na Wataalamu wa Halmashauri twendeni kwa Wananchi tukahamasishe Sensa” alisema Mhe. Francis Komba ambaye ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji wa Korogwe na Diwani wa Kata ya Mtonga wakati wa Baraza la Madiwani. Mhe. Komba alifafanua kuwa zoezi la Sensa ni jambo la kimaendeleo hivyo Madiwani pamoja na Wataalamu wa Halmashauri wanatakiwa kushiriki pamoja kuhamasisha Wananchi waweze kuhesabiwa ili Serikali iweze kufanikisha malengo iliyojiwekea katika kuwahudumia Wananchi wake.

“Mheshimiwa Mwenyekiti maagizo yote uliyotupa tumeyapokea na tutayafanyia kazi” alisema Ndugu Frank Fuko ambaye ni Naibu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Korogwe. Ndugu Fuko alifafanua kuwa Halmashauri ya Mji wa Korogwe imejipanga vyema katika kuhakikisha inatekeleza kikamilifu zoezi la Sensa linalotajajiwa kufanyika Agosti 23, mwaka huu ili kupata takwimu halisi za Watu na Makazi kwa maendeleo ya Mji wa Korogwe na Nchi kwa ujumla.

Kwa upande mwengine, Mhe Mustafa Shengwatu ambaye ni Diwani wa Kata ya Majengo alisema “Madiwani wa Mji wa Korogwe  tayari tumeshaanza na tunaendelea na zoezi la uhamasishaji wa Sensa kwa Wananchi”. Mhe. Shengwatu alisisitiza kuwa  Madiwani wote  kwa sasa wamejiwekea mkakati  kila wanapokuwa na kikao chochote iwe ni ngazi ya Kata au  kinachohusisha Wananchi moja kwa moja ushiriki wa Sensa ni agenda mojawapo itakayozungumzwa katika kikao hicho.  

“Natoa pongezi kwa Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji wa Korogwe kwa kuwahimiza Madiwani pamoja na Wataalamu wa Halmashauri kuongeza nguvu katika uhamasishaji wa Sensa” alisema Bw. Maurice Frank ambaye ni Mwananchi wa Mji wa Korogwe aliyeshiriki katika Baraza la Madiwani la Robo ya Nne linalohitimisha mwaka mwa fedha 2021/22. Bw. Maurice alifafanua kuwa iwapo kila Diwani katika eneo lake na kila Mtaalamu wa Halmashauri kwa nafasi yake atafanya jitihada za uhamashishaji wa zoezi la Sensa kwa Wananchi, Wananchi watahamasika na watashiriki ipasavyo katika kuhesabiwa.

 

Matangazo

  • Tangazo la Kazi - Afya December 06, 2024
  • TANGAZO LA KAZI - AFYA November 26, 2024
  • ERMS OF REFERENCE FOR THE PROVISION OF CONSTRUCTION SUPERVISION CONSULTANCY SERVICES FOR URBAN INFRASTRUCTURE DEVELOPMENT IN KOROGWE TOWN UNDER THE TACTIC PROJECT March 09, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • Waratibu Elimu kata na Wali Wakuu wa Shule za Msingi za Mji wa Korogwe wajengewa uwezo wa usimamizi wa ufundishaji na Ujifunzaji.

    June 27, 2025
  • Mradi wa TACTIC kuimarisha Huduma za Usafirishaji kwa Miji 12 Tanzania.

    June 26, 2025
  • Halmashauri ya Mji wa Korogwe yaadhimisha Siku ya Wajane Duniani.

    June 23, 2025
  • Shule ya Msingi Kwamngumi yalima Hekari mbili za Mahindi

    June 19, 2025
  • Angalia Zote

Video

Video Zaidi

Kurasa Muhimu

  • Ukodishaji wa Ukumbi
  • Ukasanyaji wa Taka

Tovuti Zinazohusiana

  • TOVUTI YA SERIKALI
  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • MKOA TANGA
  • TUME YA AJIRA
  • PPRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Korogwe Tanga Tanzania

    S.L.P: 615 Korogwe

    Simu: 0272650050

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@korogwetc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright©2018 Korogwe Town Council. All rights reserved.