Bi. Sharifa Wanja Afisa Elimu Awali na Msingi amefungua mafunzo ya siku tatu kwa Maafisa Elimu kata, Maafisa ustawi wa jamii ,Walimu wakuu pamoja na wenyeviti wa kamati za Shule kwa niaba ya Mkurugenzi Halmashauri ya mji wa Korogwe. Lengo kuu la Mafunzo hayo ni kuwapitisha Washiriki wa Mafunzo katika dhana ya Elimu Jumuishi. Mafunzo hayo yalitolewa na wadhibiti ubora kutoka Halmashauri ya mji wa korogwe chini ya udhamini wa Mradi wa Shule Bora.Mafunzo hayo yalifanyika katika ukumbi wa Shule ya Msingi Boma Mei 29 (Mwaka huu). Katika ufunguzi wa mafunzo hayo, afisa elimu msingi alieleza kuwa ujumuishi sio tu kuangalia wanafunzi wenye mahitaji maalum bali ni kuangalia ujumuishi wa kila mwanafunzi kwa hali yake inayomwezesha kukamilisha mzunguko mzima wa elimu yake kwa kuangalia jamii, familia anayotoka ikiwemo upatikanaji wa mahitaji muhimu kama chakula, mavazi na malazi.
Watoa mafunzo hayo ni Wadhibbiti ubora kutoka Halmashauri ya Mji wa Korogwe walibainisha Shule ambazo zimekumbwa na changamoto ya mdondoko katika Halmashauri ya Mji wa Korogwe ni pamojana Shule ya Msingi Kwamsisi na Shule ya Msingi Kwamndolwa.
Kwa upande mwingine Mwezeshaji wa Mafunzo hayo Bw. Kennedy Magumba Kabula alisema “ili kuondokana na tatizo hili la mdondoko wa Shule lazima Tathmini ifanyike kwa Shule hizo zilizobainika pamoja na kuandaa mpango kazi wa kurekebisha changamoto hizo. Naye Bi. Salome Mgalla Mwezeshaji wa Mafunzo ambaye pia ni Mdhibiti ubora wa Shule Halmashauri ya Mji wa Korogwe alifafanua kipengele cha kuandaa mpango rekebishi pamoja na kufanya Tathmini jumuishi Shuleni kwa kuzingatia mahitaji ya Wanafunzi kwa wote
Korogwe Tanga Tanzania
S.L.P: 615 Korogwe
Simu: 0272650050
Simu ya Kiganjani:
Barua Pepe: info@korogwetc.go.tz
Copyright©2018 Korogwe Town Council. All rights reserved.