• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Mji wa Korogwe
Halmashauri ya Mji wa Korogwe

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Korogwe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Afya
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi waJamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Mazingira na Udhibiti Taka Ngumu
    • Vitengo
      • Tehama na Uhusiano
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
    • Mifugo
    • Kilimo
  • Huduma Zetu
    • Za afya
    • Kielimu
    • Za Maji
    • Za kilimo
    • Mifugo
    • Huduma za watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Elimu, afya,uchumi na maji
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Picha za Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

Mbunge wa Jimbo la Korogwe Mjini atembelea miradi ya maendeleo

Posted on: January 22nd, 2022

Mbunge wa Jimbo la Korogwe Mjini atembelea miradi ya maendeleo

Mbunge wa Jimbo la Korogwe Mjini Mhe. Dkt. Alfred Kimea akiambatana pamoja na Kamati ya Fedha ya Halmashauri ya Mji wa Korogwe ametembelea miradi ya Ujenzi wa Vituo vya Afya inayotekelezwa kwa fedha za tozo za miamala ya simu pamoja na miradi ya Ujenzi wa Madarasa inayotekelezwa kwa Fedha za Uviko 19. Ukaguzi huo wa miradi ya maendeleo umefanyika January 22, mwaka huu katika maeneo mbalimbali ya Mji wa Korogwe.

Ziara ya Mbunge wa Jimbo la Korogwe Mjini pamoja na Kamati ya Fedha ya Halmashauri ya Mji wa Korogwe ilitembelea Mradi wa Ujenzi wa Madarasa katika Shule ya Sekondari Nyerere Memorial iliyopo Kata ya Manundu. Miradi mingine ni Ujenzi wa Kituo cha Afya cha Mgombezi kilichopo Kata ya Mgombezi pamoja na Mradi wa Ujenzi wa Kituo cha Afya cha Kwamsisi kilichopo Kata ya Kwamsisi.

“Natoa pongezi kwa uongozi wa Halmashauri ya Mji wa Korogwe kwa usimamizi mzuri wa ujenzi wa Madarasa” alisema Mhe. Dkt. Alfred Kimea wakati akikagua Mradi wa Ujenzi wa Madarasa Matatu katika Shule ya Sekondari ya Nyerere Memorial. Mhe. Dkt. Kimea alifafanua kuwa ni vyema fedha zilizoelekezwa kwenye miradi husika zikakamilisha miradi kwa wakati ili miradi hiyo iweze kuwanufaisha walengwa waliokusudiwa.

“Natoa shukrani kwa Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan kwa kutupatia fedha kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali” alisema Mhe. Francis Komba ambaye ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji wa Korogwe na Diwani wa Kata ya Mtonga wakati wa ziara ya ukaguzi wa Miradi ya maendeleo. Mhe. Komba alifafanua kuwa ili miradi ya maendeleo iweze kudumu  kwa muda mrefu ni vyema jamii inayozunguka mradi husika iweze kushirikishwa katika  ujenzi ili wawe sehemu ya ulinzi wa maradi wao.

Nae Bw. Mohamed Amri ambaye ni Mwananchi wa Kata ya Mgombenzi na pia ni Katibu wa Ujenzi wa Mradi wa Kituo cha Afya cha Mgombezi alitoa shukrani kwa Mbunge wa Jimbo la Korogwe Mjini Mhe. Dkt. Alfred Kimea na Kamati nzima ya Fedha ya Halmashauri ya Mji wa Korogwe kwa kututembelea ujenzi wa miradi ya maendeleo ili kuona jinsi miradi hiyo ilivyotekelezwa.

Matangazo

  • Tangazo la Kazi - Afya December 06, 2024
  • TANGAZO LA KAZI - AFYA November 26, 2024
  • ERMS OF REFERENCE FOR THE PROVISION OF CONSTRUCTION SUPERVISION CONSULTANCY SERVICES FOR URBAN INFRASTRUCTURE DEVELOPMENT IN KOROGWE TOWN UNDER THE TACTIC PROJECT March 09, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • Waratibu Elimu kata na Wali Wakuu wa Shule za Msingi za Mji wa Korogwe wajengewa uwezo wa usimamizi wa ufundishaji na Ujifunzaji.

    June 27, 2025
  • Mradi wa TACTIC kuimarisha Huduma za Usafirishaji kwa Miji 12 Tanzania.

    June 26, 2025
  • Halmashauri ya Mji wa Korogwe yaadhimisha Siku ya Wajane Duniani.

    June 23, 2025
  • Shule ya Msingi Kwamngumi yalima Hekari mbili za Mahindi

    June 19, 2025
  • Angalia Zote

Video

Video Zaidi

Kurasa Muhimu

  • Ukodishaji wa Ukumbi
  • Ukasanyaji wa Taka

Tovuti Zinazohusiana

  • TOVUTI YA SERIKALI
  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • MKOA TANGA
  • TUME YA AJIRA
  • PPRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Korogwe Tanga Tanzania

    S.L.P: 615 Korogwe

    Simu: 0272650050

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@korogwetc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright©2018 Korogwe Town Council. All rights reserved.