Mji wa Korogwe wakamilisha mradi wa ujenzi wa madarasa
Mpaka kufikia Januari 9 Mwaka huu, Tarehe ambayo Shule zote za Msingi na Sekondari hapa Nchini zinafunguliwa kwaajili ya kuanza Mhula mpya wa Masomo. Halmashauri ya Mji wa Korogwe tayari imeshakamilisha Mradi wa Ujenzi wa Mdarasa Kumi na Moja katika Shule za Sekondari. Mradi huo wenye thamani ya Shilingi Milioni 220, fedha zake zilizotolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa lengo la kupunguza uhaba wa Madarasa katika Shule za Sekondari hapa nchini.
“Kukamilika kwa Mradi wa Ujenzi wa Madarasa Kumi na Moja katika Shule za Sekondari kutasaidia kuongeza idadi ya Wanafunzi wanaotarajia kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka huu” alisema Bi. Charity Sichona ambaye ni Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Korogwe. Bi. Charity alifafanua kuwa Halmashauri ya Mji wa Korogwe imejipanga vyema kuhakikisha kila Mwanafunzi aliyechaguliwa kujiunga na Kidato cha Kwanza anapata nafsi ili kufikia lengo la Serikali.
“Madarasa yote yamejengwa kwa viwango kwa kuzingatia vigezo vyote vya Serikali vilivyoainishwa” alisema Bw. Richard Pantaleo ambaye ni Mhandisi kutoka Idara ya Ujenzi katika Halmashauri ya Mji wa Korogwe. Bw. Pantaleo alifafanua kuwa Shule zilizonufaika na Mradi wa Ujenzi wa Madarasa hayo ni pamoja na Shule ya Sekondari Semkiwa Madarasa Sita, Shule ya Sekondari Nyerere Madarasa Matatu na Shule ya Sekondari Kimweri madarsa Mawili.
Kwa upande mwengine, Bi. Mariamu Mohamed ambaye ni Mkazi wa Mji wa Korogwe anayeishi jirani na Shule ya Sekondari Semkiwa alitoa shukrani kwa serikali kwa kusema " Tunatoa pongezi kwa Mama Samia ( Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan) kwa kutujengea madarasa, madarasa haya yatasaidia Watoto wetu kujiunga kwa wingi katika Shule za Sekondari".
Korogwe Tanga Tanzania
S.L.P: 615 Korogwe
Simu: 0272650050
Simu ya Kiganjani:
Barua Pepe: info@korogwetc.go.tz
Copyright©2018 Korogwe Town Council. All rights reserved.