• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Mji wa Korogwe
Halmashauri ya Mji wa Korogwe

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Korogwe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Afya
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi waJamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Mazingira na Udhibiti Taka Ngumu
    • Vitengo
      • Tehama na Uhusiano
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
    • Mifugo
    • Kilimo
  • Huduma Zetu
    • Za afya
    • Kielimu
    • Za Maji
    • Za kilimo
    • Mifugo
    • Huduma za watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Elimu, afya,uchumi na maji
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Picha za Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

Mji wa Korogwe watangaza fursa za uwekezaji

Posted on: October 22nd, 2019

                Mji wa Korogwe watangaza fursa za uwekezaji

Halmashauri ya Mji wa Korogwe imetangaza fursa za uwekezaji katika hatua za  kukuza uchumi wa kati na kuunga mkono jitihada za Mh. John Pombe Magufuli  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuelekea uchumi wa viwanda hapa nchini. Fursa hizi za uwekezaji zilitangazwa Oktoba 22, mwaka huu wakati wa mkutano wa Baraza la biashara la wilaya ya Korogwe  katika ukumbi wa hoteli ya Korogwe Executive Lounge uliopo eneo la Kwamkole.

Akizungumzia fursa hizi ndugu Ramadhani Sekija afisa kilimo wa Halmashauri ya Mji wa Korogwe kwa niaba ya Mkurugenzi alisema milango iko wazi kwa wawekezaji kuja kuwekeza katika Mji wa Korogwe ambapo wameandaa mazingira mazuri na yenye tija kwa wawekezaji. Ndugu Sekija alianisha maeneo ya uwekezaji kama vile kilimo cha umwagiliaji, kilimo cha matunda na mbogamboga, ufugaji wa ng’ombe wa maziwa, ufugaji wa nyuki, viwanda, ujenzi wa hoteli za kitalii pamoja na elimu.

Nae ndugu Farijala Msangi ambaye ni afisa biashara wa Halmashauri ya Mji wa Korogwe alisema kuna fursa nyingi za kiuchumi ambapo wawekezaji mbalimbali wanaweza kuzichangamkia. Ndugu Msangi alisema kuna eneo kubwa la kilimo cha umwagiliaji, ambapo hekta 520 eneo la mahenge , hekta 210 eneo la Kwamngumi na hekta 420 eneo la Lwengera. Pia alizungumzia kilimo cha matunda na mbogamboga na kusema kuwa kuna ardhi ya kutosha katika maeneo ya Ngombezi, Mtonga, Old Korogwe pamoja na Kwamsisi.

Katika Sekta za viwanda, ndugu Msangi alisema katika Mji wa Korogwe yapo maeneo ya kutosha kwa ajili ya viwanda vidogo, vya kati na vikubwa ambapo kuna mita za mraba 9000 eneo la Old Korogwe na hekta 2000 eneo la Ngombezi. Hata hivyo aliwatoa hofu wawekezaji kuhusu malighafi na kusema  kuna malighafi za kutosha kutoka wilaya za jirani vilevile Mji wa Korogwe ni lango kuu la kupitisha bidhaa mbalimbali kutoka mikoa ya kaskazini hivyo kuwa na uhakika na malighafi za kutosha.

Akizungumzia fursa za Elimu ndugu Msangi alisema kuwa Mji wa Korogwe unakua kwa kasi na kuna uhitaji mkubwa wa taasisi za elimu  kuanzia elimu ya awali hadi chuo kikuu. Katika eneo la Old Korogwe kumetengwa eneo la ekari 45 kwa ajili ya shule na vyuo vya kati na ekari 77  kwajili ya vyuo vikuu. Kwa upande mwingine Mh. Hillary Ngonyani ambaye ni mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji wa Korogwe alitoa wito kwa wenyeji wa Korogwe na watanzania wote kuchangamkia fursa ya viwanja kwa ajili ya makazi na biashara vilivyopo eneo la Bagamoyo.

Matangazo

  • Tangazo la Kazi - Afya December 06, 2024
  • TANGAZO LA KAZI - AFYA November 26, 2024
  • ERMS OF REFERENCE FOR THE PROVISION OF CONSTRUCTION SUPERVISION CONSULTANCY SERVICES FOR URBAN INFRASTRUCTURE DEVELOPMENT IN KOROGWE TOWN UNDER THE TACTIC PROJECT March 09, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • Waratibu Elimu kata na Wali Wakuu wa Shule za Msingi za Mji wa Korogwe wajengewa uwezo wa usimamizi wa ufundishaji na Ujifunzaji.

    June 27, 2025
  • Mradi wa TACTIC kuimarisha Huduma za Usafirishaji kwa Miji 12 Tanzania.

    June 26, 2025
  • Halmashauri ya Mji wa Korogwe yaadhimisha Siku ya Wajane Duniani.

    June 23, 2025
  • Shule ya Msingi Kwamngumi yalima Hekari mbili za Mahindi

    June 19, 2025
  • Angalia Zote

Video

Video Zaidi

Kurasa Muhimu

  • Ukodishaji wa Ukumbi
  • Ukasanyaji wa Taka

Tovuti Zinazohusiana

  • TOVUTI YA SERIKALI
  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • MKOA TANGA
  • TUME YA AJIRA
  • PPRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Korogwe Tanga Tanzania

    S.L.P: 615 Korogwe

    Simu: 0272650050

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@korogwetc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright©2018 Korogwe Town Council. All rights reserved.