• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Mji wa Korogwe
Halmashauri ya Mji wa Korogwe

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Korogwe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Afya
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi waJamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Mazingira na Udhibiti Taka Ngumu
    • Vitengo
      • Tehama na Uhusiano
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
    • Mifugo
    • Kilimo
  • Huduma Zetu
    • Za afya
    • Kielimu
    • Za Maji
    • Za kilimo
    • Mifugo
    • Huduma za watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Elimu, afya,uchumi na maji
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Picha za Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

Mji wa Korogwe watoa Mkopo wenye thamani ya Shilingi Milioni 97

Posted on: January 11th, 2023

Mji wa Korogwe watoa Mkopo wenye thamani ya Shilingi Milioni 97

Halmaashauri ya Mji wa Korogwe katika Mwaka wa Fedha 2022/ 23 imetoa mkopo wenye thamani ya Shilingi Milioni Tisini na Saba kwa Vikundi Kumi na Sita vya Wanawake, Vijana na Watu wenye ulemavu. Mkopo huo ni sehemu ya Asilimia Kumi ya Mapato ya ndani na ikiwa pia ni agizo la Kisheri. Mgeni rasmi katika utoaji wa Mkopo huo alikua Mbunge wa Jimbo la Korogwe Mjini Mhe. Dkt Alfred Kimea. Halfa ya utoaji Mkopo huo imefanyika Januari 11, Mwaka huu katika Uwanja vya Sokoni uliopo Kata ya Manundu.

Vikundi vilivyonufaika na Mkopo wa kiasi cha Shilingi Milioni Tisini na Saba kutoka Halmashauri vinajihusisha na shughuli mbalimbali za Kiuchumi ikijumuisha Uuzaji wa nafaka , Usafirishaji wa abiria  na mizigo, pamoja na Kilimo cha matunda na mbogamboga. Shughuli nyingine ni Ufugaji wa kuku, Ubunifu wa Mavazi ( ushonaji wa nguo) pamoja na Kazi mbalimbali za ufundi.

“Serikali imedhamiria kwa dhati kuwawezesha Kiuchumi Watu wa Hali ya chini ikijumuisha pia na Watu wenye ulemavu” alisema Mhe. Dkt. Alfred Kimea ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Korogwe Mjini wakati akikabidhi Hundi ya Shilingi Milioni Tisini na Saba kwa wahufaika wa Mkopo huo. Mhe. Dkt. Kimea alisisitiza kuwa Wanawake, Vijana na Watu wenye ulemavu wachangamkie fursa ya Mikopo ya Halmashauri ambayo ina masharti nafuu kwa lengo la kujikwamua kiuchumi.

“ Halmashauri imefanya jitihada za utoaji  wa Mkopo  wa  Asilimia Kumi kwa kuzingatia usawa ikihusisha Vikundi kutoka Kata zote za Mji wa Korogwe” alisema Bw. Frank Fuko ambaye ni Kaimu Mukurugenzi wa  Halmashauri ya Mji wa Korogwe. Bw. Fuko alifafanua kuwa Halmashauri itaendelea na jitihada za utoaji wa Mikopo kadri fedha zitakapopatikana.

Kwa upande mwengine, Bi. Rehema Letara ambaye ni Kaimu Afisa Maendeleo ya Jamii wa Halmashauri ya Mji wa Korogwe alitoa nasaha kwa wanufaika wa Mikopo kwa kusema “ Wanufaika wote wa Mikopo hakikisheni mnarejesha mikopo kwa wakati ili Wananchi wengine waweze kunufaika na mikopo hiyo” Nae Bw. Mwanga Ntandu ambaye ni mnufaika wa Mikopo mwenye uoni haifu  alitoa shukrani kwa kusema  “Watu wenye ulemavu tunatoa shukrani kwa Halmashauri na Serikali kwa ujumla kwa kutupatiwa mikopo yenye masharti nafuu,  mikopo hii itatusaidia  kujikwamua kiuchumi” .

Matangazo

  • Tangazo la Kazi - Afya December 06, 2024
  • TANGAZO LA KAZI - AFYA November 26, 2024
  • ERMS OF REFERENCE FOR THE PROVISION OF CONSTRUCTION SUPERVISION CONSULTANCY SERVICES FOR URBAN INFRASTRUCTURE DEVELOPMENT IN KOROGWE TOWN UNDER THE TACTIC PROJECT March 09, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • Halmashauri ya Mji wa Korogwe imepokea Chanjo na Vifaa wezeshi

    July 11, 2025
  • Idara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi Halmashauri ya Mji wa Korogwe imepokea Chanjo ya Mifugo.

    July 10, 2025
  • Mkurugenzi wa Mji wa Korogwe atembelea Ujenzi wa Miradi ya Maendeleo.

    July 10, 2025
  • Serikali yatatua Changamoto ya Makazi kwa Watumishi wa Umma

    July 04, 2025
  • Angalia Zote

Video

Video Zaidi

Kurasa Muhimu

  • Ukodishaji wa Ukumbi
  • Ukasanyaji wa Taka

Tovuti Zinazohusiana

  • TOVUTI YA SERIKALI
  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • MKOA TANGA
  • TUME YA AJIRA
  • PPRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Korogwe Tanga Tanzania

    S.L.P: 615 Korogwe

    Simu: 0272650050

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@korogwetc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright©2018 Korogwe Town Council. All rights reserved.