Mkuu wa Wilaya ya Korogwe ahamashisha upandaji wa Miti
Kuelekea kilele cha Sherehe ya Maadhimisho ya Miaka 60 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar Aprili 26, Mwaka huu. Mkuu wa Wilaya ya Korogwe Mhe. William Mwakilema amepanda Miti ikiwa ni maadhimisho ya Miaka 60 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar. Zoezi hilo la upandaji wa Miti mbalimbali lilifanyika Aprili 23, Mwaka huu katika Viwanja vya Nyumba ya Mkuu wa Wilaya ya Korogwe pamoja na Nyumba ya Katibu Tawala wa Wilaya ya Korogwe.
Zoezi hilo la upandaji wa Miti lilishirikisha pia Katibu Tawala wa Wilaya ya Korogwe Bi. Mwanaidi Rajabu, Maafisa Tarafa kutoka Tarafa zilizopo Wilaya ya Korogwe, Wafanyakazi wa Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Korogwe, Wataalamu kutoka Halmashauri ya Mji wa Korogwe Pamoja na Viongozi wa Chama cha Mapinduzi (CCM) kutoka Wilaya ya Korogwe Mjini pamoja na Korogwe Vijijini.
“Naomba tuadhimishe miaka 60 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar kwa upandaji wa miti katika maeneo yetu, zoezi hili la upandaji wa miti liwe endelevu kwa manufaa yetu na vizazi vijavyo” alisema Mkuu wa Wilaya ya Korogwe Mhe. William Mwakilemwa wakati wa zoezi la upandaji wa Miti kuadhimisha Miaka 60 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar. Mhe. Mwakilema alisisitiza kuwa ni vyema Wananchi wakati wa upandaji wa miti, wapande miti yenye tija itakayowanufaisha kwa matunda Pamoja na Mbao.
Maadhimisho ya Miaka 60 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar Katika Wilaya ya Korogwe yanaadhimishwa kwa upandaji wa miti, Usafi wa Mazingira, Mdahalo juu Matunda ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar Pamoja na Michezo mbalimbali. Uratibu wa zoezi lote la Maadhimisho litakuwa chini ya Mkuu wa Wilaya ya Korogwe akishirikisha Halmashauri ya Wilaya ya Korogwe, Mji wa Korogwe Pamoja na Taasisi zote za Serikali zilizopo Wilaya ya Korogwe.
Korogwe Tanga Tanzania
S.L.P: 615 Korogwe
Simu: 0272650050
Simu ya Kiganjani:
Barua Pepe: info@korogwetc.go.tz
Copyright©2018 Korogwe Town Council. All rights reserved.