• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Mji wa Korogwe
Halmashauri ya Mji wa Korogwe

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Korogwe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Afya
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi waJamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Mazingira na Udhibiti Taka Ngumu
    • Vitengo
      • Tehama na Uhusiano
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
    • Mifugo
    • Kilimo
  • Huduma Zetu
    • Za afya
    • Kielimu
    • Za Maji
    • Za kilimo
    • Mifugo
    • Huduma za watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Elimu, afya,uchumi na maji
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Picha za Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

Mwenyekiti, Mkurugenzi wa Mji wa Korogwe watembelea miradi ya elimu na afya

Posted on: April 27th, 2022

Mwenyekiti, Mkurugenzi wa Mji wa Korogwe watembelea miradi ya elimu na afya

Mwnyekiti wa Halmashauri ya Mji wa Korogwe Mhe. Francis Komba akiambatana na Mkurugenzi pamoja na Kamati ya Fedha na Utawala ya Halamshauri hiyo wametembelea miradi ya afya na elimu ikiwa ni hatua ya ukaguzi wa miradi katika kuhitimisha kipindi cha Robo ya Tatu katika mwaka wa Fedha 2021/22. Ziara hiyo ya kutembelea miradi katika maeneo mbalimbali ya Mji wa Korogwe imefanyika Aprili 27, mwaka huu.

Katika zira hiyo,  Kamati ya Fedha na Utawala walitembelea mradi wa  Ujenzi wa jengo la Wagojwa wa Dharura katika Hospitali ya Mji wa Korogwe (Magunga ) wenye thamani ya Shilingi Milioni Mia Tatu,  Mradi wa Ujenzi wa Kituo cha Afya cha Kwamsisi wenye thamani ya Shilingi Milioni Miambili na Hamsini pamoja na  Mradi wa Ujenzi wa Shule ya Sekondari ya Bagamoyo wenye thamani ya Shilingi Milioni Mia Nne.

Pamoja na kutembelea miradi ya elimu na afya, Kamati ya Fedha na Utawala pia ilitembelea Miradi mingine ukiwepo  Mradi wa Karakana ya Sevia wenye thamani ya Shilingi Milioni Sita, Mradi huo wa Karakana ya Sevia unaomilikiwa na Vijana ambao wanaojishughulisha na ufundi wa magari. Mradi mwengine ni ufungaji wa Kamera za CCTV katika Kituo cha Mabasi cha Balozi John Kijazi wenye thamani ya Shilingi Milioni Tano.

“Mhandisi wa Halmashauri hakikisha ujenzi wa Jengo la Wagonjwa wa dharura linakua na ubora wa hali ya juu  na kukidhi vigezo vyote kwa mujibu wa ramani uliyopewa” alisema Mhe. Francis Komba ambaye ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji wa Korogwe na Diwani wa Kata ya Mtonga wakati akifanya ukaguzi wa Jengo la Wagonjwa wa Dharura katika Hospitali ya Mji wa Korogwe (Magunga). Mhe. Francis Komba alisisitiza kuwa Wakandarasi  wote waliopewa ujenzi wa miradi  ya Halmashauri wahakikishe wanakamilisha  miradi yote ndani ya muda uliopangwa.

“Halmashauri imejipanga vyema kuhakikisha kila Mkandarasi aliyepewa kandarasi ya ujenzi anatimiza majukumu yake kwa ufanisi, Mkandarasi yoyote atakayekabidhi jengo lenye mapungufu hatomaliziwa fedha zake mpaka arekebishe mapungufu yaliyojitokeza katika jengo lake” alisema Bi. Bernadetha ambaye ni Mchumi wa Halmashauri ya Mji wa Korogwe anayemuwakilisha Mkurugenzi. Bi. Bernadetha alisisitiza kuwa Mkandarasi yoyote atakayejihisi analegalega katika kutimiza majukumu yake ni vyema akajisalimisha mapema kwa maslahi ya Halmashauri na Serikali kwa ujumla.

“ Wananchi wa Mji wa Korogwe tuanatoa shukrani kwa Halmashauri ya Mji wa Korogwe na Serikali kwa ujumla kwa kufanikisha mradi wa Ujenzi wa Jengo la Wagojwa wa Dharura  katika Hospitali ya Mji wa Korogwe (Magunga), Jengo litakapokamilika litasaidi kutoa matibabu ya dharura kwa Wananchi wa Mji  Korogwe na maeneo ya jirani” alisema Bw.  Juma Stambuli ambaye ni Mwananchi wa Kata ya Magunga katika Mji wa Korogwe.

Matangazo

  • Tangazo la Kazi - Afya December 06, 2024
  • TANGAZO LA KAZI - AFYA November 26, 2024
  • ERMS OF REFERENCE FOR THE PROVISION OF CONSTRUCTION SUPERVISION CONSULTANCY SERVICES FOR URBAN INFRASTRUCTURE DEVELOPMENT IN KOROGWE TOWN UNDER THE TACTIC PROJECT March 09, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • Waratibu Elimu kata na Wali Wakuu wa Shule za Msingi za Mji wa Korogwe wajengewa uwezo wa usimamizi wa ufundishaji na Ujifunzaji.

    June 27, 2025
  • Mradi wa TACTIC kuimarisha Huduma za Usafirishaji kwa Miji 12 Tanzania.

    June 26, 2025
  • Halmashauri ya Mji wa Korogwe yaadhimisha Siku ya Wajane Duniani.

    June 23, 2025
  • Shule ya Msingi Kwamngumi yalima Hekari mbili za Mahindi

    June 19, 2025
  • Angalia Zote

Video

Video Zaidi

Kurasa Muhimu

  • Ukodishaji wa Ukumbi
  • Ukasanyaji wa Taka

Tovuti Zinazohusiana

  • TOVUTI YA SERIKALI
  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • MKOA TANGA
  • TUME YA AJIRA
  • PPRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Korogwe Tanga Tanzania

    S.L.P: 615 Korogwe

    Simu: 0272650050

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@korogwetc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright©2018 Korogwe Town Council. All rights reserved.