• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Mji wa Korogwe
Halmashauri ya Mji wa Korogwe

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Korogwe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Afya
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi waJamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Mazingira na Udhibiti Taka Ngumu
    • Vitengo
      • Tehama na Uhusiano
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
    • Mifugo
    • Kilimo
  • Huduma Zetu
    • Za afya
    • Kielimu
    • Za Maji
    • Za kilimo
    • Mifugo
    • Huduma za watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Elimu, afya,uchumi na maji
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Picha za Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

Wilaya ya Korogwe yafanya maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani

Posted on: May 1st, 2022

Wilaya ya Korogwe yafanya maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani

Wilaya ya Korogwe imeungna na Maeneo mengine hapa Nchini na Ulimwengu kwa ujumla katika kuadhimisha Siku ya Wafanyakazi Duniani. Siku ambayo huadhimishwa Ulimwenguni kote kila ifikapo Mei 01, ya kila mwaka.   Siku ya Wafanyakazi Duaniani mwaka huu Wilayani Korogwe iliadhimishwa kwa Wafanyakazi kushiriki katika Maandamano ya Wafanyakazi pamoja na Michezo mbalimbali. Maadhimisho hayo ya Siku ya Wanyakazi Duniani yalifanyika katika Viwanja vya Chuo cha Ualimu Korogwe (Korogwe TTC).

Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani yaliyofanyika Wilayani Korogwe yalishirikisha   Viongozi mbalimbali pamoja na Wafanyakazi kutoka  Sekta za Umma pamoja na Binafsi  huku wakiwakilisha vyama vyao vya Wafanyakazi kikiwapo Chama cha  CWT, TALGWU, TIPAU, TUGHE  pamoja na Chama cha TUICO. Kauli mbiu ya Mwaka huu kwa hapa Nchini ni ”Mishahara na Maslahi bora kwa Wafanyakazi ndio kilio chetu,  Kazi Iendelee”.  Mgeni rasmi katika Maadhimisho hayo  ya Kiwilaya alikua Mkuu wa Wilaya ya Korogwe Mhe. Basilla Mwanukuzi.

“Wakurugenzi wote, hakikisheni mnatatua changamoto za mafao ya likizo pamoja utoaji wa motisha za Wafanyakazi” alisema  Mkuu wa Wilaya ya Korogwe Mhe. Basilla Mwanukuzi  wakati akizungumza na Wafanyakazi walioshiriki katika Siku ya Wafanyakazi Duniani katika Viwanja vya Korogwe TTC. Mhe. Mwanukuzi alifafanua kuwa pamoja na changamoto ndogondogo zilizopo katika maeneo ya kazi, Wafanyakazi ni vyema kufanya kazi kwa bidii pamoja na kuimarisha mshikamo katika maeneo ya kazi.

“Tunatoa pongezi kwa Mheshimiwa Rais kwa kuongeza jitihada za kutatua kero za Wafanyakazi hapa nchini”alisema Bi. Pilli Mdoe ambaye ni Katibu wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT) Wilayani Korogwe wakati akisoma Risala ya Siku ya Wafanyakazi Duniani katika Viwanja vya Korogwe TTC. Bi. Pilli alisisitiza kuwa anaimani kubwa salamu za kero za wafanyakazi hapa Nchi zitamfikia Mheshimiwa Rais na kero hizo atazipatia ufumbuzi katika kuhakikisha wafanyakazi wanaboreshewa maslahi bora katika maeneo ya kazi.

Katika hatua nyengine, Bi. Pili Mdoe alitoa pongezi kwa Viongozi mbalimbali pamoja na Wafanyakazi wa Vyama vyote vya Wafanyakazi kwa kushiriki katika  Maadhimisho hayo ya Siku ya Wafanyakazi Duniani kwa ngazi ya Wilaya. Nao Wafanyakazi walioshiriki katika Maadhimisho hayo walitoa shukrani kwa Viongozi vya Vyama vya Wafanyakazi na Serikali kwa ujumla kwa kufanikisha Maadhimisho hayo yenye lengo la kuimarisha umoja na mshikamano wa Wafanyakazi katika kudai maslahi bora katika maeneo yao ya  kazi.

Matangazo

  • Tangazo la Kazi - Afya December 06, 2024
  • TANGAZO LA KAZI - AFYA November 26, 2024
  • ERMS OF REFERENCE FOR THE PROVISION OF CONSTRUCTION SUPERVISION CONSULTANCY SERVICES FOR URBAN INFRASTRUCTURE DEVELOPMENT IN KOROGWE TOWN UNDER THE TACTIC PROJECT March 09, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • Halmashauri ya Mji wa Korogwe imepokea Chanjo na Vifaa wezeshi

    July 11, 2025
  • Idara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi Halmashauri ya Mji wa Korogwe imepokea Chanjo ya Mifugo.

    July 10, 2025
  • Mkurugenzi wa Mji wa Korogwe atembelea Ujenzi wa Miradi ya Maendeleo.

    July 10, 2025
  • Serikali yatatua Changamoto ya Makazi kwa Watumishi wa Umma

    July 04, 2025
  • Angalia Zote

Video

Video Zaidi

Kurasa Muhimu

  • Ukodishaji wa Ukumbi
  • Ukasanyaji wa Taka

Tovuti Zinazohusiana

  • TOVUTI YA SERIKALI
  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • MKOA TANGA
  • TUME YA AJIRA
  • PPRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Korogwe Tanga Tanzania

    S.L.P: 615 Korogwe

    Simu: 0272650050

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@korogwetc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright©2018 Korogwe Town Council. All rights reserved.