Wilaya ya Korogwe yajipanga kupambana na ugonjwa wa Corona
Mkuu wa Wilaya ya Korogwe Mh. Kissa Kasongwa ameitisha kikao chini ya kamati ya huduma za afya ya msingi ( PHC) kujadili mpango mkakati wa kudhibiti ugonjwa wa Corona katika Wilaya ya Korogwe. Kikao hicho kilifanyika Machi 16, mwaka huu katika ukumbi wa mikutano uliopo Chuo cha ualimu Korogwe.
Akizungumzai mkakati wa kupambana na maradhi ya Corona Mh. Kissa Kasongwa ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Korogwe alisema “ njia pekee ya kupambana na maradhi ya Corona ni kuhamasishana katika jamii kuzingatia usafi binafsi pamoja na kuepuka mikusanyo isiyo na ulazima”. Mh. Kasongwa aliendelea kufafanua kuwa kwa sasa Wilaya ya Korogwe ni salama na haina maambukizi ya maradhi ya Corona.
Katika hatua nyingine Mh. Kasongwa alisema kuwa tayari Wilaya ya Korogwe wameshatenga eneo maalumu kwa ajili ya watu watakaothibitika kuwa na maambukizi ya ugonjwa wa Corona. Pia alizipongeza Halmashauri ya Mji wa Korogwe pamoja na ya Wilaya ya Korogwe kwa kutenga bajeti kwa ajili ya mapambano dhidi ya ugojwa huo.
Nae Dkt. Elizabeth Nyema ambaye ni Mganga mkuu wa Halmashauri ya Mji wa Korogwe pamoja na Dkt. Frank Chiduo ambaye ni Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Wilaya ya Korogwe walisema kuwa tayari wameshaanza kutoaa elimu ya mapambano dhidi ya maradhi ya Corona kuanzia ngazi za Vijiji, Mitaa hadi katika taasisi za serikali pamoja taasisi binafsi. Dkt. Nyema alisema “ni vyema wananchi kuhakikisha wananawa mikono kwa maji yanayotiririka mara kwa mara”.
Kwa upande mwingine Ndugu Cristopher Magafu ambaye ni Afisa afya kutoka Halmashauri ya Mji wa Korogwe alisema “ ugonjwa wa Corona huweza kuwapata watu wote wakike na kiume hivyo kila mwananchi anatakiwa kuchukua tahadhari ya kujikinga” Ndugu Magafu alitoa ushauri kwa jamii kwa kusema kuwa mtu yoyote anaweza kutoa taarifa kwenye huduma za kituo cha afya anapoona mtu mwenye dalili za ugojwa wa Corona au kupiga simu namba 0800110124 au 0800110125.
Korogwe Tanga Tanzania
S.L.P: 615 Korogwe
Simu: 0272650050
Simu ya Kiganjani:
Barua Pepe: info@korogwetc.go.tz
Copyright©2018 Korogwe Town Council. All rights reserved.