Madiwani wa Halmashauri za Korogwe Mji,Wilaya ya Muheza pamoja na Wilaya ya Korogwe wapatiwa Mafunzo ya kuwajengea uwezo katika majukumu yao. Mafunzo hayo ya siku tatu yana lengo la kuwajengea uwezo Madiwani katika utendaji kazi kwa kuzingatia sheria, kanuni, taratibu na miongozo wa Serikali za Mitaa yamefanyika Januari 29, 2026 na yanatarajia kumalizika Januari 31, 2026 katika ukumbi wa GMCC ulipo Kata ya Bagamoyo Halmashauri ya Mji Korogwe.
Akizungumza katika ufunguzi wa mafunzo ya Siku tatu ya Madiwani wa Halmashauri hizo Mwakilishi wa Mkuu wa Wilaya ya Korogwe, Bw. Alex Mhando ambaye ni Afisa Tarafa wa Korogwe amewaasa Waheshimiwa Madiwani kujenga wajibu wa pamoja katika uongozi, Kuwa Wasimamizi wazuri katika kutatua migogoro na si kuwa vyanzo vya migogoro.
Aidha amesema kuwa “Tupo hapa kwa Karama ya Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan” hivyo tuwe chachu ya kutii sheria, kanuni na mamlaka ili kulinda heshima ya Nchi Yetu na kuleta tabasabu kwa Wananchi wetu.
Katika mafunzo hayo ya Siku tatu Waheshimiwa Madiwani wa Halmashauri ya Korogwe Mji,Wilaya na Muheza wamepata mafunzo kuhusu Utawala Bora, Sheria za Serikali za Mitaa na kanuni za uendeshaji wa vikao, lengo likiwa kuwajengea uwezo katika utekelezaji wa Majukumu yao ya kila siku.
Mafunzo ya Madiwani Katika Halmashauri ya hizo yametolewa na wataalam kutoka Chuo cha Serikali za Mitaa Hombolo pamoja na Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa.
Korogwe Tanga Tanzania
S.L.P: 615 Korogwe
Simu: 0272650050
Simu ya Kiganjani:
Barua Pepe: info@korogwetc.go.tz
Copyright©2018 Korogwe Town Council. All rights reserved.