• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Mji wa Korogwe
Halmashauri ya Mji wa Korogwe

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Korogwe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Afya
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi waJamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Mazingira na Udhibiti Taka Ngumu
    • Vitengo
      • Tehama na Uhusiano
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
    • Mifugo
    • Kilimo
  • Huduma Zetu
    • Za afya
    • Kielimu
    • Za Maji
    • Za kilimo
    • Mifugo
    • Huduma za watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Elimu, afya,uchumi na maji
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Picha za Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

Madiwani, Wataalamu wa Halmashauri watakiwa kusimamia miradi kwa ufanisi

Posted on: November 3rd, 2021

Madiwani, Wataalamu wa Halmashauri watakiwa kusimamia miradi kwa ufanisi

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji wa Korogwe Mhe. Francis Komba amewataka Madiwani pamoja na Wataalamu wa Halmashauri ya Mji wa Korogwe kusimamia miradi ya maendeleo kwa ufanishi ili iweze kuleta jita iliyokusudiwa na Serikali. Maelekezo hayo aliyatoa wakati wa Kikao cha Baraza la Madiwani kilichofanyika Novemba 03, mwaka huu katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Mji wa Korogwe.  Kikao hicho cha Baraza la Madiwani kilikaliwa kwa lengo la kuhitimisha Robo ya Kwanza kwa Mwaka wa fedha 2021/22.

“Madiwani, pamoja na Wataalamu wa Halmashauri simamieni miradi ya maendeleo kwa ufanisi ili iweze kuleta tija kwa Wananchi” alisema Mhe. Frascis Komba ambaye ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji wa Korogwe na Diwani wa Kata ya Mtonga wakati wa Kikao cha Baraza la Madiwani. Mhe. Komba alifafanua kuwa endapo miradi ya maendeleo kama vile miradi ya elimu na afya ikisimamiwa kwa ufanisi, miradi hiyo inaweza kujengwa  kwa kiwango na kumalizika kwa wakati.

Katika hatua nyingine Mhe. Francis Komba alisisitiza kuwa Serikali inapotoa fedha kwa ajili ya ujenzi wa miradi ya maendeleo, fedha hiyo inapaswa kwenda katika eneo husika ili Serikali iweze kutimiza lengo lake.  Iwapo Madiwani au Wataalamu wa Halmashauri wakienda kinyume na maelekezo ya mradi husika Serikali itachukua hatua kali za kisheria.  Mhe Komba alisema “wenzetu wa TAKUKURU mmewasikia wakitupatia elimu ya usimamizi wa miradi ya maendeleo, natumaini kila mmoja wetu elimu ile ataifanyia kazi”

“Sisi kama Halmashauri tumejipanga vyema katika usimamizi wa miradi ya maendeleo” alisema Ndugu Nicodemus Bei ambaye ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Korogwe. Ndugu Bei alifafanua kuwa licha ya kupokea fedha zinazotolewa na Serikali kuu kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo, Halmashauri pia imeanzisha mradi wa utengenezaji  wa matofali  kwa fedha za ndani kwa lengo la kuongeza vyanzo vya mapato katika Halmashauri hiyo.

Nae Ndugu Fulgence Komba ambaye ni Katibu wa Mbunge wa Jimbo la Korogwe Mjini Mhe. Dkt. Alfred Kimea aliishukuru Serikali kwa kuipatia fedha Halmashauri ya Mji wa Korogwe kwaajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo. Ndugu Komba alisisitiza kuwa jukumu la usimamizi wa miradi ya maendeleo haliwahusu Madiwani na Watalaamu wa Halmashauri pekeyao, Wananchi pia wanatakiwa kushiriki ili kuhakikisha miradi inakamilika kwa wakati.

Matangazo

  • Tangazo la Kazi - Afya December 06, 2024
  • TANGAZO LA KAZI - AFYA November 26, 2024
  • ERMS OF REFERENCE FOR THE PROVISION OF CONSTRUCTION SUPERVISION CONSULTANCY SERVICES FOR URBAN INFRASTRUCTURE DEVELOPMENT IN KOROGWE TOWN UNDER THE TACTIC PROJECT March 09, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • Waratibu Elimu kata na Wali Wakuu wa Shule za Msingi za Mji wa Korogwe wajengewa uwezo wa usimamizi wa ufundishaji na Ujifunzaji.

    June 27, 2025
  • Mradi wa TACTIC kuimarisha Huduma za Usafirishaji kwa Miji 12 Tanzania.

    June 26, 2025
  • Halmashauri ya Mji wa Korogwe yaadhimisha Siku ya Wajane Duniani.

    June 23, 2025
  • Shule ya Msingi Kwamngumi yalima Hekari mbili za Mahindi

    June 19, 2025
  • Angalia Zote

Video

Video Zaidi

Kurasa Muhimu

  • Ukodishaji wa Ukumbi
  • Ukasanyaji wa Taka

Tovuti Zinazohusiana

  • TOVUTI YA SERIKALI
  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • MKOA TANGA
  • TUME YA AJIRA
  • PPRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Korogwe Tanga Tanzania

    S.L.P: 615 Korogwe

    Simu: 0272650050

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@korogwetc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright©2018 Korogwe Town Council. All rights reserved.