• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Mji wa Korogwe
Halmashauri ya Mji wa Korogwe

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Korogwe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Afya
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi waJamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Mazingira na Udhibiti Taka Ngumu
    • Vitengo
      • Tehama na Uhusiano
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
    • Mifugo
    • Kilimo
  • Huduma Zetu
    • Za afya
    • Kielimu
    • Za Maji
    • Za kilimo
    • Mifugo
    • Huduma za watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Elimu, afya,uchumi na maji
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Picha za Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

Mkurugenzi wa Mji wa Korogwe atembelea mradi wa ujenzi wa kituo cha afya

Posted on: November 4th, 2021

Mkurugenzi wa Mji wa Korogwe atembelea mradi wa ujenzi wa kituo cha afya

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Korogwe Ndugu Nicodemus Bei akiambatana pamoja na Mchumi wa Halmashauri hiyo Bi. Bernadetha January ametembelea mradi wa ujenzi wa Kituo cha Afya cha Mgombezi uliopo Kata ya Mgombezi. Lengo la kutembelea mradi huo wa Kituo cha Afya ni kukagua maendeleo ya ujenzi na kujionea hatua ulipofikia. Ziara ya kutembelea mradi wa ujenzi wa kituo hicho cha afya imefanyika Novemba 04, mwaka huu.

“Kituo hiki kitakapokamilika kitawasaidia Wananchi wa Mgombezi na maeneo ya jirani kupata huduma za afya karibu na maeneo yao” alisema Ndugu Nicodemus Bei ambaye ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Korogwe wakati wa ukaguzi wa mradi huo. Ndugu Bei alifafanua kuwa Wananchi wote wanaishi maeneo ya pembeni ya Mji wa Korogwe ikiwapo Kata ya Mgombezi Halmashauri imeweka mkakati wa kuwapatia huduma za afya jirani na maeneo yao ili kuwapunguzia mwendo wa kwenda Hospitali ya Mji wa Korogwe (Magunga).

“Halmashauri ya Mji wa Korogwe tunatoa shukurani za dhati kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa kutupatia fedha za ujenzi wa Kituo cha Afya cha Mgombezi” alisema Bi. Bernadetha January ambaye ni Mchumi wa Halmashauri ya Mji wa Korogwe. Bi. Bernadetha alifafanua kuwa Serikali inatekeleza ujenzi wa Kituo cha Afya cha Mgombezi kwa gharama ya Shilingi Milioni Mia Tano na tayari Serikali imeshatoa Shilingi Milioni Mia Mbili na Hamsini za awali kwa utekelezaji wa mradi huo.

Kwa upande mwengine, Ndugu Charles Kamugisha ambaye ni Mhandisi wa Halmashauri ya Mji wa Korogwe alifafanua kuwa  Mradi wa Kituo  cha Afya cha Mgombezi utakuwa na majengo mawili, jengo la kwanza litakuwa la Mama, Baba na Mtoto na jengo la pili litakuwa la upasuaji. Kuhusu utekelezaji wa mradi huo, Ndugu Kamugisha alifafanua kuwa mradi unatakelezwa kwa muda wa miezi Minne na ujenzi ulianza rasmi Oktoba mwaka huu na utakamilika Januari 2022.

Nae Ndugu Steven Mwita ambaye ni Mwananchi wa Kata ya Mgombezi  alitoa shukrani kwa Halmashauri ya Mji wa Korogwe na Serikali kwa ujumla kwa kuwapatia mradi wa ujenzi wa Kituo cha Afya kitakachosaidia kuwapatia huduma karibu na maeneo yao.

Matangazo

  • Tangazo la Kazi - Afya December 06, 2024
  • TANGAZO LA KAZI - AFYA November 26, 2024
  • ERMS OF REFERENCE FOR THE PROVISION OF CONSTRUCTION SUPERVISION CONSULTANCY SERVICES FOR URBAN INFRASTRUCTURE DEVELOPMENT IN KOROGWE TOWN UNDER THE TACTIC PROJECT March 09, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • Idara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi Halmashauri ya Mji wa Korogwe imepokea Chanjo ya Mifugo.

    July 10, 2025
  • Mkurugenzi wa Mji wa Korogwe atembelea Ujenzi wa Miradi ya Maendeleo.

    July 10, 2025
  • Serikali yatatua Changamoto ya Makazi kwa Watumishi wa Umma

    July 04, 2025
  • Serikali yatatua Changamoto ya Makazi kwa Watumishi wa Umma

    July 04, 2025
  • Angalia Zote

Video

Video Zaidi

Kurasa Muhimu

  • Ukodishaji wa Ukumbi
  • Ukasanyaji wa Taka

Tovuti Zinazohusiana

  • TOVUTI YA SERIKALI
  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • MKOA TANGA
  • TUME YA AJIRA
  • PPRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Korogwe Tanga Tanzania

    S.L.P: 615 Korogwe

    Simu: 0272650050

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@korogwetc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright©2018 Korogwe Town Council. All rights reserved.