• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Mji wa Korogwe
Halmashauri ya Mji wa Korogwe

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Korogwe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Afya
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi waJamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Mazingira na Udhibiti Taka Ngumu
    • Vitengo
      • Tehama na Uhusiano
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
    • Mifugo
    • Kilimo
  • Huduma Zetu
    • Za afya
    • Kielimu
    • Za Maji
    • Za kilimo
    • Mifugo
    • Huduma za watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Elimu, afya,uchumi na maji
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Picha za Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

Wananchi wa Mji wa Korogwe wahimizwa kujiunga na Elimu ya Watu Wazima

Posted on: October 13th, 2022

Wananchi wa Mji wa Korogwe wahimizwa kujiunga na Elimu ya Watu Wazima

Wananchi wa Mji wa Korogwe walioshindwa kupata elimu katika utaratibu maalumu kutokana na changamoto mbalimbali wameshauriwa kujiunga na Elimu ya Watu Wazima ili kuepukana na changamoto ya kutojua Kuandika, Kusoma na Kuhesabu.  Ushauri huo umetolewa na Diwani wa Kata ya Kwamsisi Mhe. Nassoro Mohamed aliyekua Mgeni rasmi wakati wa Maadhimisho ya Juma la Elimu ya Watu Wazima katika Halmashuri ya Mji wa Korogwe. Maadhimisho hayo yalifanyika Oktoba 13, Mwaka huu katika Shule ya Msingi Manundu Mazoezi.

“Twendeni tukawahimize Wananchi waliokosa elimu katika utaratibu maalumu wajiunge na Elimu ya Watu Wazima ili kuepukana na changamoto ya kutojua Kuandika, Kusoma na Kuhesabu” alisema Mhe. Nassoro Mohamed ambaye ni Diwani wa Kata ya Kwamsisi wakati wa Maadhimisho ya Juma la Elimu ya Watu Wazima. Mhe. Nassoro alisisitiza kuwa Wananchi watakaojiunga na Elimu ya Watu Wazima watanufaika na elimu katika nyanja mbalimbali ikiwa ni  pamoja na kupata ujuzi wa fani za kila aina kulingana na uhitaji wao.

“Halmashauri ya Mji wa Korogwe imejipanga vyema kuhakikisha inatoa Elimu ya Watu Wazima kwa kila kundi kulingana na uhitaji wao” alisema Bw. Aseri Mshana ambaye ni Afisa Elimu ya Watu Wazima katika Halmashauri ya Mji wa Korogwe. Bw. Mshana alifafanua kuwa  licha ya  Halmashauri kujipanga vyema katika kuhakikisha inapunguza idadi ya watu wasiojua Kuandika, Kusoma na Kuhesabu  lakini pia  inampango wa  kuhamasisha Wananchi kupata ujuzi wa fani mbalimbali kulingana na mazingira yao ili kujikwamua kimaisha.

Kwa upande mwengine,  Wadau  wa elimu, Viongozi mbalimbali pamoja na Wananchi walioshiriki katika Maadhimisho ya Juma la Elimu Ngazi ya Halmashauri Mwaka 2022, walitoa pongezi kwa Halmashauri ya Mji wa Korogwe na Serikali kwa ujumla kwa kuwaleta  Wananchi wa Mji wa Korogwe katika Jukwaa  Moja kwa lengo la  kujadili changamoto za Elimu ya Watu Wazima na njia za kutatua changamoto hizo ili Wananchi  waweze  kwenda sambamba na maendeleo ya Kiuchumi, Kisiasa na Kijamii wakiwa na elimu ya kutosha.

Matangazo

  • Tangazo la Kazi - Afya December 06, 2024
  • TANGAZO LA KAZI - AFYA November 26, 2024
  • ERMS OF REFERENCE FOR THE PROVISION OF CONSTRUCTION SUPERVISION CONSULTANCY SERVICES FOR URBAN INFRASTRUCTURE DEVELOPMENT IN KOROGWE TOWN UNDER THE TACTIC PROJECT March 09, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • Waratibu Elimu kata na Wali Wakuu wa Shule za Msingi za Mji wa Korogwe wajengewa uwezo wa usimamizi wa ufundishaji na Ujifunzaji.

    June 27, 2025
  • Mradi wa TACTIC kuimarisha Huduma za Usafirishaji kwa Miji 12 Tanzania.

    June 26, 2025
  • Halmashauri ya Mji wa Korogwe yaadhimisha Siku ya Wajane Duniani.

    June 23, 2025
  • Shule ya Msingi Kwamngumi yalima Hekari mbili za Mahindi

    June 19, 2025
  • Angalia Zote

Video

Video Zaidi

Kurasa Muhimu

  • Ukodishaji wa Ukumbi
  • Ukasanyaji wa Taka

Tovuti Zinazohusiana

  • TOVUTI YA SERIKALI
  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • MKOA TANGA
  • TUME YA AJIRA
  • PPRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Korogwe Tanga Tanzania

    S.L.P: 615 Korogwe

    Simu: 0272650050

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@korogwetc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright©2018 Korogwe Town Council. All rights reserved.