• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Mji wa Korogwe
Halmashauri ya Mji wa Korogwe

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Korogwe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Afya
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi waJamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Mazingira na Udhibiti Taka Ngumu
    • Vitengo
      • Tehama na Uhusiano
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
    • Mifugo
    • Kilimo
  • Huduma Zetu
    • Za afya
    • Kielimu
    • Za Maji
    • Za kilimo
    • Mifugo
    • Huduma za watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Elimu, afya,uchumi na maji
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Picha za Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

Katibu Tawala Wilaya ya Korogwe atoa msaada Hospitali ya Lutindi

Posted on: November 23rd, 2021

Katibu Tawala Wilaya ya Korogwe  atoa msaada Hospitali ya Lutindi

Kuelekea maadhimisho ya miaka 60 ya uhuru wa Tanganyika ambapo kilele chake kitafanyika Desemba 9, mwka huu Katibu Tawala wa Wilaya ya Korogwe Bi. Rahel Mhando akiwa pamoja na Kamati ya maandalizi ya maadhimisho ya  Miaka 60 ya uhuru wa Tanganyika  Novemba 23, mwaka huu ameshiriki kazi za kijamii pamoja na kutoa  msaada wa vifaa mbalimbali katika Hospitali ya afya ya akili ya Lutindi  iliyopo Kata ya Lutindi Wilayani Korogwe .

Maadhimisho ya miaka 60 ya uhuru wa Tanganyika mwaka huu yanakwenda sambamba na utoaji wa misaada kwa makundi maalumu pamoja na kushiriki kazi mbalimbali za kijamii. Katika ziara ya kutembelea Hospitali ya Lutindi Bi. Rahel Mhando  ambaye ni Katibu Tawala wa Wilaya ya Korogwe  akiwa pamoja na  Kamati ya maaandalizi ya maadhimisho ya miaka 60 ya uhuru wa Tanganyika ameshiriki katika usafi wa mazingira  pamoja na kutoa msaada wa  vifaa mbalimbali kama vile mchele, unga wa sembe, sukari, mafuta ya kupikia pamoja na sabuni.

“Katika kuelekea maadhimisho ya miaka 60 ya uhuru wa Tanganyika, serikali imeona ni jambo la busara kumipatia msaada  ndugu zetu mliopo hapa ili tuweze kusheherekea kwa pamoja sikukuu ya uhuru wa nchi yetu” alisema Bi. Rahel Mhando ambaye ni Katibu Tawala wa Wilaya Korogwe wakati akitoa msada kwa wagojwa wa afya ya akili katika Hospitali ya Lutindi. Bi. Rahel alifafanua kuwa Serikali itaendeleza utamaduni wa kuwajulia hali wagonjwa waliopo Hospitali ya Lutindi ili kuwafariji katika kipindi kigumu wananchopitia.

“Natoa shukani kwa kamati ya maandalizi ya  maadhimisho ya miaka 60 ya uhuru wa Tanganyika na Serikali kwa ujumla kwa kutupatia msaada katika hosptitali yetu” alisema  Dkt Marwa Katyetye ambaye ni mganga mkuu wa Hospitali ya afya ya akili ya Lutindi. Dkt Marwa  alifafanua kuwa wagonjwa wa afya ya akili wanapotembelewa na ndugu, jamaa na marafiki wanapata faraja na kujiona pia ni sehemu ya jamii hivyo kupata uchangamfu wa akili.

Nae Mhe. Imanueli Mng’ong’oso ambaye ni Diwani wa Kata ya Lutindi alisema “  sisi wananchi tunaozunguka hospitali hii ya Lutindi, wagojwa wa afya ya akili waliopo Hospitalini hapa ni ndugu zetu bila ya kujali anatoka sehemu gani,  wananchi wa Lutindi tunatoa shukrani za  dhati kwa serikali kwa kuwapatia msaada ndugu zetu”.

Nao  Wananchi wa Lutindi walioshirikia  katika usafi wa mazingira pamoja na kuwajuli hali wagonjwa wakiambatana na Katibu wa Wilaya ya Korogwe walitoa shukrani kwa  Viongozi wa Wilaya ya Korogwe na Serikali kwa ujumla kwa kutembelea Hospitali ya Lutindi.

  

Matangazo

  • Tangazo la Kazi - Afya December 06, 2024
  • TANGAZO LA KAZI - AFYA November 26, 2024
  • ERMS OF REFERENCE FOR THE PROVISION OF CONSTRUCTION SUPERVISION CONSULTANCY SERVICES FOR URBAN INFRASTRUCTURE DEVELOPMENT IN KOROGWE TOWN UNDER THE TACTIC PROJECT March 09, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • Waratibu Elimu kata na Wali Wakuu wa Shule za Msingi za Mji wa Korogwe wajengewa uwezo wa usimamizi wa ufundishaji na Ujifunzaji.

    June 27, 2025
  • Mradi wa TACTIC kuimarisha Huduma za Usafirishaji kwa Miji 12 Tanzania.

    June 26, 2025
  • Halmashauri ya Mji wa Korogwe yaadhimisha Siku ya Wajane Duniani.

    June 23, 2025
  • Shule ya Msingi Kwamngumi yalima Hekari mbili za Mahindi

    June 19, 2025
  • Angalia Zote

Video

Video Zaidi

Kurasa Muhimu

  • Ukodishaji wa Ukumbi
  • Ukasanyaji wa Taka

Tovuti Zinazohusiana

  • TOVUTI YA SERIKALI
  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • MKOA TANGA
  • TUME YA AJIRA
  • PPRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Korogwe Tanga Tanzania

    S.L.P: 615 Korogwe

    Simu: 0272650050

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@korogwetc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright©2018 Korogwe Town Council. All rights reserved.