• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Mji wa Korogwe
Halmashauri ya Mji wa Korogwe

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Korogwe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Afya
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi waJamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Mazingira na Udhibiti Taka Ngumu
    • Vitengo
      • Tehama na Uhusiano
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
    • Mifugo
    • Kilimo
  • Huduma Zetu
    • Za afya
    • Kielimu
    • Za Maji
    • Za kilimo
    • Mifugo
    • Huduma za watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Elimu, afya,uchumi na maji
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Picha za Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

Mkuu wa Wilaya ya Korogwe akabidhi Mkopo wa Milioni 152 kwa Makundi Maalumu

Posted on: March 31st, 2022

Mkuu wa Wilaya ya Korogwe akabidhi Mkopo wa Milioni 152 kwa Makundi Maalumu

Mkuu wa Wilaya ya Korogwe Mhe. Basilla Mwanaukuzi amekabidhi Mkopo wa Shilingi Milioni 152 kwa Wanawake, Vijana na Watu wenye ulemavu waliopo Mji wa Korogwe. Mkopo huo wa Shilingi Milioni 152 waliokabidhiwa Wanawake, Vijana na Watu wenye ulemavu ulitolewa na Halmashauri ya Mji wa Korogwe ambao ni Asilimia Kumi zinazotokana na makusanyo ya ndani ya Halmashauri hiyo. Warsha ya kukabidhi mkopo huo imefanyika Machi 31, mwaka huu katika Kijiji cha Kwakombo kilichopo Mji wa Korogwe.

“Natoa wito kwa Maafisa Kilimo, Maendeleo ya Jamii pamoja na Maafisa Biashara waweze kutoa ushauri kwa wanufaika wa mikopo ili waweze kutumia mikopo hiyo kwa manufaa” alisema Mhe. Basilla Mwanukuzi ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Korogwe wakati akukabidhi mkopo wa Shilingi Milioni 152 kwa Wanawake, Vijana na Watu Wenye ulemavu. Mhe. Mwanukuzi alisisitiza kuwa ni jambo la busara watu wote walionufaika na mkopo huo waweze kurejesha mkopo kwa wakati ili Vikundi vyengine viweze kunufaikia na mkopo huo.

“Halmashauri ya Mji wa Korogwe itaendelea kutoa mkopo wa Asilimia Kumi kwa Wanawake, Vijana na Watu wenye ulemavu kadri fedha zinapopatikana” alisema Bi. Bernadetha January ambaye ni Mchumi wa Halmashauri ya Mji wa Korogwe aliyemuwakilisha Mkurugenzi. Bi. Bernadetha alifafanua kuwa utoaji wa mikopo wa Makundi Maalumu sio takwa la kiutashi bali ni agizo la kisheria, hivyo Halmashauri itaendeleo na jitihata za kutoa mkopo kwa Makundi Maalumu kwa lengo la kuhakikisha Makundi hayo nayajiimarisha kiuchumi.

Kwa upande mwengine, Bi. Chariy Sichona ambaye ni Afisa Maandeleo ya Jamii wa Halmashauri ya Mji wa Korogwe alifafanua kuwa mkopo wa Shilingi Milioni 152 uliotolewa na Halmashauri umenufaisha Vikundi Ishirini na Sita. Katika Vikundi hivyo Wanawake wamepatiwa Shilingi Milioni 72,500,000, Vijana Shilingi Milioni 49,500,000 na Watu wenye ulemavu Shilingi Milioni 30,000,000.  Bi. Charity alifafanua kuwa mkopo huo wa Shilingi Milioni 152 ulijumuisha utoaji wa Fedha  taslimu, Bajaji, Mashine mbalimbali pamoja na Pikikipi.

“Kwa niaba ya Vikundi vyote natoa shukrani kwa Halmashauri ya Mji wa Korongwe na Serikali kwa ujumla ya Mhe. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kututhamini watu wa Makundi Maalumu na kutupatia mkopo kwa lengo la kujikwamua kiuchumi” alisema Mzee Athumani Selemani ambaye ni Mlemavu wa miguu na mnufaika wa mkopo wa Bajaji wakati akitoa shukrani kwa Mkuu wa Wilaya ya Korogwe kwa niaba ya Vikundi vyote ambavyo ni wanufaika wa mkopo.

Matangazo

  • Tangazo la Kazi - Afya December 06, 2024
  • TANGAZO LA KAZI - AFYA November 26, 2024
  • ERMS OF REFERENCE FOR THE PROVISION OF CONSTRUCTION SUPERVISION CONSULTANCY SERVICES FOR URBAN INFRASTRUCTURE DEVELOPMENT IN KOROGWE TOWN UNDER THE TACTIC PROJECT March 09, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • Serikali yatatua Changamoto ya Makazi kwa Watumishi wa Umma

    July 04, 2025
  • Serikali yatatua Changamoto ya Makazi kwa Watumishi wa Umma

    July 04, 2025
  • Serikali yatatua Changamoto ya Makazi kwa Watumishi wa Umma.

    July 04, 2025
  • Mwakilishi wa Mkuu wa Wilaya ameyataka mashirika yasiyo ya kiserikali kufuata Sheria na miongozo ya Serikali

    July 01, 2025
  • Angalia Zote

Video

Video Zaidi

Kurasa Muhimu

  • Ukodishaji wa Ukumbi
  • Ukasanyaji wa Taka

Tovuti Zinazohusiana

  • TOVUTI YA SERIKALI
  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • MKOA TANGA
  • TUME YA AJIRA
  • PPRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Korogwe Tanga Tanzania

    S.L.P: 615 Korogwe

    Simu: 0272650050

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@korogwetc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright©2018 Korogwe Town Council. All rights reserved.