• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Mji wa Korogwe
Halmashauri ya Mji wa Korogwe

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Korogwe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Afya
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi waJamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Mazingira na Udhibiti Taka Ngumu
    • Vitengo
      • Tehama na Uhusiano
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
    • Mifugo
    • Kilimo
  • Huduma Zetu
    • Za afya
    • Kielimu
    • Za Maji
    • Za kilimo
    • Mifugo
    • Huduma za watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Elimu, afya,uchumi na maji
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Picha za Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji wa Korogwe atembelea vyanzo vya mapato

Posted on: November 26th, 2021

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji wa Korogwe atembelea vyanzo vya mapato 

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji wa Korogwe Mhe. Francis Komba akiambatana pamoja na Kamati ya Fedha ya Halmashauri hiyo ametembelea vyanzo vya mapato vya Halmashauri kwa lengo la kuangalia mafanikio pamoja na changamoto zinazojitokeza wakati wa ukusanyaji mapato.  Hatua hiyo ya kutembelea vyanzo vya mapato katika  ni moja ya utekelezaji wa mkakati ya kuimarisha ukusanyaji wa mapato katika Halmashauri. Ziara hiyo ya kukagua vyanzo mbalimbali vya mapato katika Mji wa Korogwe imefanyika Novemba 26, mwaka huu.

Katika ziara hiyo ya kutembelea vyanzo vya mapato, Mwenyekiti wa Halmashauri pamoja na Kamati ya Fedha ya Halmashauri hiyo walitembelea vyanzo mbalimbali vya mapato.  Vyanzo hivyo vya mapato ni pamoja na Machinjio ya ng’ombe na mbuzi, Stendi ya John Kijazi, Soko la Kilole pamoja na  Geti la ushuru wa mazao ya kilimo. Vyanzo vingine ni Soko la Old Korogwe, Stendi ya zamani, pamoja na Maeneo ya wazi.

“Madiwani pamoja na Wataalamu wa Halmashauri tushirikiane kwa pamoja katika kuongeza mapato ya Halmashauri” alisema Mhe. Francis Komba ambaye ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji wa Korogwe na Diwani wa Kata ya Mtonga. Mhe. Komba alifafanua kuwa ili Halmashauri iweze kusonga mbele kimaendeleo inahitajka kuwa na mapato ya kutosha, hivyo ni muda muafaka Madiwani pamoja na Wataalamu wa Halmashauri kuimarisha vyanzo vilivyopo pamoja na kubuni vyanzo vipya ili kuongeza mapato ya Halmashauri.

Katika hatua nyengine, Mhe. Francis Komba alisisitiza kuwa mtu yeyote atakayejaribu kuvujisha mapato ya Halmashauri bila kujali yeye ni nani, sheria itachukua mkondo wake ikiwa ni pamoja na kupelekwa mahakamani. Hata hivyo Mhe. Komba alitoa wito kwa Madiwani pamoja na Wataalamu wa Halmashauri kuwaelimishe Wananchi juu ya umuhimu wa Kolipa kodi katika vitega uchumi vya Halmashauri au kulipa ushuru katika maeneo mbalimbali. Iwapo Wananchi wataelimishwa vyema watalipa kodi au ushuru bila ya changamoto yoyote.

“Mheshimiwa Mwenyekiti ushauri wote uliotoa tumeupokea, sisi kama Wataalamu wa Halmashauri tumejipanga vyema kuhakikisha tunaongeza mapato katika Halmashauri yetu” alisema Ndugu Gaspa Mtui ambaye ni Kaimu Mueka Hazina wa Halmashauri ya Mji wa Korogwe. Ndugu Mtui alifafanua kuwa katika jitihada za kuongeza vyanzo vipya vya mapato, Halmashauri tayari imeshaanzisha Kiwanda cha kufyatulia tofali za saruji. Kiwanda hicho kinauwezo wa kufyatua tofali Elfu Nne kwa siku moja.

 

Matangazo

  • Tangazo la Kazi - Afya December 06, 2024
  • TANGAZO LA KAZI - AFYA November 26, 2024
  • ERMS OF REFERENCE FOR THE PROVISION OF CONSTRUCTION SUPERVISION CONSULTANCY SERVICES FOR URBAN INFRASTRUCTURE DEVELOPMENT IN KOROGWE TOWN UNDER THE TACTIC PROJECT March 09, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • Waratibu Elimu kata na Wali Wakuu wa Shule za Msingi za Mji wa Korogwe wajengewa uwezo wa usimamizi wa ufundishaji na Ujifunzaji.

    June 27, 2025
  • Mradi wa TACTIC kuimarisha Huduma za Usafirishaji kwa Miji 12 Tanzania.

    June 26, 2025
  • Halmashauri ya Mji wa Korogwe yaadhimisha Siku ya Wajane Duniani.

    June 23, 2025
  • Shule ya Msingi Kwamngumi yalima Hekari mbili za Mahindi

    June 19, 2025
  • Angalia Zote

Video

Video Zaidi

Kurasa Muhimu

  • Ukodishaji wa Ukumbi
  • Ukasanyaji wa Taka

Tovuti Zinazohusiana

  • TOVUTI YA SERIKALI
  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • MKOA TANGA
  • TUME YA AJIRA
  • PPRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Korogwe Tanga Tanzania

    S.L.P: 615 Korogwe

    Simu: 0272650050

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@korogwetc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright©2018 Korogwe Town Council. All rights reserved.