Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi Mh. Jaji wa Rufaa Jacobs Mwambegele amewataka wa Wananchi wa Jimbo la Korogwe Mjini kujitokeza kwa wingi kwenye zoezi la Uboreshaji wa Taaarifa zao pamoja kutoa taarifa za watu waliofariki na wasio raia wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania ili waondolewe kwenye zoezi la uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura. Mh. Jaji Mwambegele alitoa kauli hiyo wakati wa kupokea taarifa ya zoezi zima la uboreshaji wa daftari la kudumu la mpiga kura kutoka kwa Afisa Mwandishikishaji wa Jimbo la Korogwe Mjini Bi. Mwashabani Mrope Mei 19, 2025 katika Ofisi ya Afisa Mwandikishaji Jimbo la Korogwe Mjini.
Kwa upande mwingine Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi Mh. Jaji wa Rufaa Jacobs Mwambegele amempongeza Afisa Mwandikishaji wa Jimbo la Korogwe Mjini kwa kazi kubwa anayoisimamia na zoezi la Uboreshaji linaenda vizuri. Kisha Jaji Mwambegele alipata wasaa wa kutembelea Vituo vya Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la mpiga kura ili kuona hali halisi ya zoezi linavyokwenda. Vituo alivyotembelea Mh. Jaji Jacobs Mwambegele ni pamoja na kituo cha Shule ya Msingi Mazoezi kilichopo Kata ya Manundu, Kituo cha Chuo cha Ualimu Korogwe (TTC) na Kituo cha Ofisi ya Mtendaji wa kata ya Majengo.
Korogwe Tanga Tanzania
S.L.P: 615 Korogwe
Simu: 0272650050
Simu ya Kiganjani:
Barua Pepe: info@korogwetc.go.tz
Copyright©2018 Korogwe Town Council. All rights reserved.