• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Mji wa Korogwe
Halmashauri ya Mji wa Korogwe

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Korogwe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Afya
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi waJamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Mazingira na Udhibiti Taka Ngumu
    • Vitengo
      • Tehama na Uhusiano
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
    • Mifugo
    • Kilimo
  • Huduma Zetu
    • Za afya
    • Kielimu
    • Za Maji
    • Za kilimo
    • Mifugo
    • Huduma za watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Elimu, afya,uchumi na maji
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Picha za Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

Ujenzi wa barabara ya Hoza-Ramia Korogwe mjini wakamilika kwa asilimia 92

Posted on: April 18th, 2019

Mradi wa ujenzi wa barabara Hoza-Ramia yenye urefu wa mita 690, unatarajiwa kukamilika mwishoni mwa mwezi huu kwani mradi uko katika hatua za mwisho za uwekaji wa lami.

Kaimu Mhandisi wa Ujenzi wa Halmashauri ya Mji Korogwe Ndugu Dionis Ernest amesema “mradi huu umeanza tarehe 2/8/2018 ambao msimamizi wake ni NIMETA CONSULT LTD ambapo fedha za mradi huo zimetolewa na Benki ya Dunia  chini ya mradi wa ULGSP”.

Ameongeza kuwa mpaka kukamilika kwa mradi wa ujenzi wa barabara hiyo kutagharimu jumla ya Tsh 843,063,358.00 pamoja na VAT ambapo barabara hiyo inajengwa kwa kiwango cha lami ngumu ambayo itakuwa na uwezo wa  kupitisha magari yenye uzito mkubwa, huku kazi ya kuweka lami ikitarajiwa kuanza siku chache kuanzia sasa.

Pia amesema shughuli inayoendelea kwa sasa ni kumalizia ujenzi wa barabara pamoja na ujenzi wa mifereji ili kuwezesha maji kupita kwa urahisi na pia kutakuwa na ufungaji wa taa za barabarani zitakazowezesha watumiaji wa barabara ya Hoza-Ramia kuona wanapokuwa wakitumia barabara hiyo.

Mkaguzi wa vifaa vya ujenzi wa NIMETA CONSULT LTD Bw. Lazaro Mveyange amesema “barabara imekamilika kwa 92% na kwa upande wa mifereji pia imekamilika kwa 97% kilichobaki ni kujengea vizuri kipande kidogo kilichobaki ili kuruhusu maji kupita vizuri”.

Aidha Bw. Mveyange amesema kuwa changamoto wanayokumbana nayo ni uelewa wa watumiaji wa barabara kwani hawafati alama zilizowekwa za kuzuia watu kupita au vyombo vya usafiri kwenye eneo la mradi hivyo kusababisha kuharibu sehemu ambazo ziko katika ujenzi.

Mfanyabiashara na mkazi wa eneo hili ambapo kuna ujenzi wa barabara Bw. Suleiman Ramadhan Msofe amesema “nashukuru kuona barabara hii inajengwa kwa kiwango cha lami na sisi wakazi wa hapa tutakuwa tunaenda sokoni huku tukitembea kwenye lami tofauti na mwanzoni”.

Bw. Msofe amesema “mtaa utafunguka kibiashara kwani tumesikia kutakuwa na ufungaji wa taa za barabarani ambazo zitatuwezesha kufanya shughuli za kibiashara mpaka usiku na huu ujenzi wa mifereji utasaidia maji kupita kwa urahisi hivyo hayatasumbua kama ilivyokuwa zamani ambapo maji yalikuwa yanakosa njia sahihi zakupita na kupelekea kuingia katika makazi ya watu, pia kutakuwa na usalama mkubwa kutokana na uwepo wa taa hizo watakazoweka kwenye barabara”

Ujenzi  huu wa barabara ya Hoza-Ramia  yenye urefu wa mita 690 utasaidia kufanya watumia vyombo vya usafiri na watumiaji wengine kufika kwa wakati sehemu mbalimbali wanazoenda bila tatizo lolote na pia kufungua fursa za biashara kwa wananchi wote wa Mji wa Korogwe na viunga vyake.                                     

Matangazo

  • Tangazo la Kazi - Afya December 06, 2024
  • TANGAZO LA KAZI - AFYA November 26, 2024
  • ERMS OF REFERENCE FOR THE PROVISION OF CONSTRUCTION SUPERVISION CONSULTANCY SERVICES FOR URBAN INFRASTRUCTURE DEVELOPMENT IN KOROGWE TOWN UNDER THE TACTIC PROJECT March 09, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • Halmashauri ya Mji wa Korogwe imepokea Chanjo na Vifaa wezeshi

    July 11, 2025
  • Idara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi Halmashauri ya Mji wa Korogwe imepokea Chanjo ya Mifugo.

    July 10, 2025
  • Mkurugenzi wa Mji wa Korogwe atembelea Ujenzi wa Miradi ya Maendeleo.

    July 10, 2025
  • Serikali yatatua Changamoto ya Makazi kwa Watumishi wa Umma

    July 04, 2025
  • Angalia Zote

Video

Video Zaidi

Kurasa Muhimu

  • Ukodishaji wa Ukumbi
  • Ukasanyaji wa Taka

Tovuti Zinazohusiana

  • TOVUTI YA SERIKALI
  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • MKOA TANGA
  • TUME YA AJIRA
  • PPRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Korogwe Tanga Tanzania

    S.L.P: 615 Korogwe

    Simu: 0272650050

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@korogwetc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright©2018 Korogwe Town Council. All rights reserved.