• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Mji wa Korogwe
Halmashauri ya Mji wa Korogwe

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Korogwe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Afya
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi waJamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Mazingira na Udhibiti Taka Ngumu
    • Vitengo
      • Tehama na Uhusiano
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
    • Mifugo
    • Kilimo
  • Huduma Zetu
    • Za afya
    • Kielimu
    • Za Maji
    • Za kilimo
    • Mifugo
    • Huduma za watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Elimu, afya,uchumi na maji
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Picha za Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

Ujenzi wa vyumba vya madarasa na vyoo katika shule ya msingi Boma na Zung’nat wafikia hatua ya ukamilikaji

Posted on: April 11th, 2019

Mradi wa ujenzi wa madarasa  mawili(2) na vyoo katika Shule ya Msingi Boma na Zung’nat zilizopo katika Halmashauri ya Mji Korogwe zimefikia katika hatua nzuri, ambapo madarasa na vyoo vipo katika hatua ya mwisho ya ukamilishwaji.

Mradi huo ambao umegharimu Tsh  milioni 44 na laki 4 zikiwa ni za ujenzi wa Shule ya Misingi Boma, huku Tsh milioni 46 na laki 6 zikiwa ni kwaajili ya ujenzi wa Shule ya Msingi Zung’nat.

 Fedha hizo ambazo zimetolewa na mpango wa lipa kulingana na matokeo (EP4R) kupitia Serikali ya awamu ya tano chini ya Rais  Dk. John Pombe Magufuli katika jitihada za kupunguza uhaba wa madarasa na vyoo ili kuwafanya wanafunzi kusoma katika mazingira bora na salama.

Afisa Elimu wa Halmashauri ya Mji Korogwe Bw. Kaoneka amesema kuwa mradi wa ujenzi wa madarasa na vyoo katika shule zote mbili, Shule ya Msingi Boma na Zung’nat unaendelea vizuri na kwamba uko katika hatua za mwisho kukamilika.

 Kwa upande wa Shule ya Msingi Boma kuna ujenzi wa madarasa mawili(2) na matundu manne ya vyoo(4), ambapo madarasa yote mawili(2) yako katika hatua ya uwekaji wa madirisha na kupiga plasta, huku vyoo vikiwa tayari na zoezi lililobaki ni uchimbaji wa mashimo ya vyoo.

 Pia katika Shule ya Msingi Zung’nat kuna ujenzi wa madarasa mawili(2) pamoja na matundu sita(6) ya vyoo, ambapo kwa upande wa madarasa yako kwenye hatua ya kupiga plasta, vyoo vimeshajengwa na vimekamilika.

Aidha ushiriki wa jamii kwa baadhi ya maeneo katika ujenzi wa madarasa na vyoo ni mdogo haswa katika ujenzi wa Shule ya Msingi Boma kulinganisha na ujenzi wa shule ya msingi Zung’nat ambapo wananchi wameshiriki kikamilifu katika kusaidia ujenzi  wa madarasa.

Jamii inashiriki katika ujenzi wa madarasa na vyoo  kwa kuchota maji, kukusanya kokoto, kuchimba msingi na kubeba maji na hivyo kusaidia kupunguza gharama na kuharakisha ujenzi.

Changamoto kubwa katika ujenzi wa madarasa na vyoo ni pamoja na uhaba wa maji hasa ukizingatia kuwa hiki ni kipindi cha kiangazi.

Bw. Kaoneka amesema ‘bado kuna uhaba wa madarasa kama watatokea wadau wengine wanaweza kutusaidia kujenga madarasa mengine’.

Mradi wa ujenzi huu wa madarasa pamoja na vyoo katika Shule ya Msingi Boma na Zung’nat unatarajiwa kukamilika mwishoni mwa mwezi huu.

Matangazo

  • Tangazo la Kazi - Afya December 06, 2024
  • TANGAZO LA KAZI - AFYA November 26, 2024
  • ERMS OF REFERENCE FOR THE PROVISION OF CONSTRUCTION SUPERVISION CONSULTANCY SERVICES FOR URBAN INFRASTRUCTURE DEVELOPMENT IN KOROGWE TOWN UNDER THE TACTIC PROJECT March 09, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • Waratibu Elimu kata na Wali Wakuu wa Shule za Msingi za Mji wa Korogwe wajengewa uwezo wa usimamizi wa ufundishaji na Ujifunzaji.

    June 27, 2025
  • Mradi wa TACTIC kuimarisha Huduma za Usafirishaji kwa Miji 12 Tanzania.

    June 26, 2025
  • Halmashauri ya Mji wa Korogwe yaadhimisha Siku ya Wajane Duniani.

    June 23, 2025
  • Shule ya Msingi Kwamngumi yalima Hekari mbili za Mahindi

    June 19, 2025
  • Angalia Zote

Video

Video Zaidi

Kurasa Muhimu

  • Ukodishaji wa Ukumbi
  • Ukasanyaji wa Taka

Tovuti Zinazohusiana

  • TOVUTI YA SERIKALI
  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • MKOA TANGA
  • TUME YA AJIRA
  • PPRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Korogwe Tanga Tanzania

    S.L.P: 615 Korogwe

    Simu: 0272650050

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@korogwetc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright©2018 Korogwe Town Council. All rights reserved.