• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Mji wa Korogwe
Halmashauri ya Mji wa Korogwe

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Korogwe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Afya
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi waJamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Mazingira na Udhibiti Taka Ngumu
    • Vitengo
      • Tehama na Uhusiano
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
    • Mifugo
    • Kilimo
  • Huduma Zetu
    • Za afya
    • Kielimu
    • Za Maji
    • Za kilimo
    • Mifugo
    • Huduma za watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Elimu, afya,uchumi na maji
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Picha za Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

Baraza la Madiwani lapitisha ujenzi wa kituo cha afya

Posted on: March 12th, 2020

Baraza la madiwani lapitisha ujenzi wa kituo cha afya

Baraza la Madiwani katika Halmashauri ya Mji wa Korogwe limepitisha Ujenzi wa Kituo cha afya katika Kata ya Kwamsisi pamoja na ununuzi wa mashine mpya ya mionzi (x-ray) kwa ajili ya Hospitali ya Mji wa Korogwe. Baraza hilo ambalo ni la robo ya pili katika  mwaka wa fedha 2019/ 2020 limefanyika Machi 12, mwaka huu katika ukumbi wa Halmashauri ya Mji wa Korogwe.

Akizungumzia mchakato huo Mh. Hillary Ngonyani ambaye ni  Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji wa Korogwe  alisema “ mpango wa ujenzi wa Kituo cha afya cha Kwamsisi ni moja ya mikakati ya Halmashauri  ya Mji wa Korogwe katika kuboresha sekta ya afya na tutaendelea na ujenzi wa vituo  katika Kata vyingine”.

 Nae Ndugu Nicodemus Bei ambaye ni  Mkurugenzi wa Mji wa Korogwe alisema kuwa Baraza la Madiwani limepitisha ujenzi wa kituo cha afya katika Kata ya Kwamasisi ili kuwapatia wananchi  huduma za afya  baada ya  baadhi ya huduma kukosekana katika zahanati ya Kwamsisi hadi Hospitali ya Mji wa Korogwe (Magunga) ambako ni mbali na eneo hilo.

Kwa upande wa  Diwani wa Kata ya Kwamsisi Mh. Nassoro Hassan alilishukuru Baraza la Madiwani kwa kupitisha mchakato wa ujenzi wa Kituo cha afya cha Kwamsisi  na alisema “ ujenzi wa kituo hiki ni jambo la faraja kwa wananchi wa kata yangu, wananchi wataweza kupata huduma za afya za huhakika kwa ukaribu zaidi’’.

Katika hatua nyingine Madiwani walipitisha ununuzi wa mashine  mpya ya mionzi (x-ray) ambayo itakuwa  ni maalumu  kwa ajili ya Hospitali ya Mji wa Korogwe (Magunga). Kupatikana kwa  mashine mpya  kutasaidia kupunguza changamoto za huduma ya mionzi baada ya mashine iliyopo kuharibika.  Nae Dkt. Elizabeth Nyema  ambaye ni Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Mji wa Korogwe alisema kuwa mashine hiyo mpya itanunuliwa kutoka Shirika la usambazaji dawa la Medical Store Depatment (MSD) kwa gharama za takribani milioni mia tatu tisini.

Matangazo

  • Tangazo la Kazi - Afya December 06, 2024
  • TANGAZO LA KAZI - AFYA November 26, 2024
  • ERMS OF REFERENCE FOR THE PROVISION OF CONSTRUCTION SUPERVISION CONSULTANCY SERVICES FOR URBAN INFRASTRUCTURE DEVELOPMENT IN KOROGWE TOWN UNDER THE TACTIC PROJECT March 09, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • Waratibu Elimu kata na Wali Wakuu wa Shule za Msingi za Mji wa Korogwe wajengewa uwezo wa usimamizi wa ufundishaji na Ujifunzaji.

    June 27, 2025
  • Mradi wa TACTIC kuimarisha Huduma za Usafirishaji kwa Miji 12 Tanzania.

    June 26, 2025
  • Halmashauri ya Mji wa Korogwe yaadhimisha Siku ya Wajane Duniani.

    June 23, 2025
  • Shule ya Msingi Kwamngumi yalima Hekari mbili za Mahindi

    June 19, 2025
  • Angalia Zote

Video

Video Zaidi

Kurasa Muhimu

  • Ukodishaji wa Ukumbi
  • Ukasanyaji wa Taka

Tovuti Zinazohusiana

  • TOVUTI YA SERIKALI
  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • MKOA TANGA
  • TUME YA AJIRA
  • PPRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Korogwe Tanga Tanzania

    S.L.P: 615 Korogwe

    Simu: 0272650050

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@korogwetc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright©2018 Korogwe Town Council. All rights reserved.