• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Mji wa Korogwe
Halmashauri ya Mji wa Korogwe

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Korogwe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Afya
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi waJamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Mazingira na Udhibiti Taka Ngumu
    • Vitengo
      • Tehama na Uhusiano
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
    • Mifugo
    • Kilimo
  • Huduma Zetu
    • Za afya
    • Kielimu
    • Za Maji
    • Za kilimo
    • Mifugo
    • Huduma za watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Elimu, afya,uchumi na maji
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Picha za Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

Kidato cha sita Korogwe Girls warudi shuleni

Posted on: June 2nd, 2020

 Kidato cha sita Korogwe Girls warudi shuleni

Wanafunzi wa kidato cha sita katika Shule ya Sekondari  Korogwe Girls wamerudi shuleni baada ya kukaa nyumbani kwa muda wa takribani miezi miwili kutokana na changamoto ya ugonjwa wa Corona (Covid – 19). Wanafunzi walianza kuwasili shuleni kuanzia Mei 30, na Shule ilifunguliwa rasmi June 1, mwaka huu baada ya agizo la Serikali kutaka wanafunzi wote wa vyuo  wapamoja na kidato cha sita warudi shuleni kuendelea na masomo.

Akizungumzia ujio wa wanafunzi Bi. Annisia Mauka ambaye ni Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Korogwe Girls alisema “uongozi wa shule pamoja na watalaamu wa afya waliopo shuleni tumejiandaa vyema  kuwapokea wanafunzi na mpaka sasa mambo yote yanakwenda vizuri”. Bi Mauka aliendelea kufafanua kuwa mpaka kufikia June 2, mwaka huu tayari wanafunzi 308 wameshawasili kati ya wanafunzi 362 waliosajiliwa.

Kwa upande wa masomo Bi Mauka alisema “tumejipanga vizuri kuwafundisha wanafunzi ili waweze kujiandaa vyema na mitihani ya kidato cha sita inayotarajiwa kuanza June 26, mwaka huu.” Pia Bi Mauka alifafanua kuwa tayari wameshatoa elimu ya kutosha kwa wanafunzi jinsi ya kujikinga na ugojwa wa Corona (Covid – 19) na vilevile  kufuata maelekezo  ya kiafya ambayo ni  kuwapima joto wanafunzi wanapowasili shuleni, wanafunzi kuvaa barakoa, kukaa mita moja kutoka meza moja hadi nyingine pamoja na kuweka maji safi tiririka na sabuni katika maeneo mbalimbali ya shule.

Nae Dr. Joyceline Sombo ambaye ni Daktari katika Zahanati ya Shule ya Korogwe Girls alisema “wanafunzi wote 308 waliwasili wako vyema baada ya kuwapima joto la mwili na matokeo kuonesha wanajoto la wastani”. Dr. Sombo alifafanua kuwa wanafunzi wana furaha ya kutosha na hawana hofu yoyote na ugonjwa wa Corona (Covid -19), hofu kubwa ya wanafunzi iko kwenye mitihani ya kumalizia masomo yao.  Kwa upande wa wanafunzi walitoa shukurani kwa uongozi wa shule na Serikali kwa ujumla kwa maandalizi mazuri pamoja na kuweka mikakati imara ya masomo.

Matangazo

  • Tangazo la Kazi - Afya December 06, 2024
  • TANGAZO LA KAZI - AFYA November 26, 2024
  • ERMS OF REFERENCE FOR THE PROVISION OF CONSTRUCTION SUPERVISION CONSULTANCY SERVICES FOR URBAN INFRASTRUCTURE DEVELOPMENT IN KOROGWE TOWN UNDER THE TACTIC PROJECT March 09, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • Waratibu Elimu kata na Wali Wakuu wa Shule za Msingi za Mji wa Korogwe wajengewa uwezo wa usimamizi wa ufundishaji na Ujifunzaji.

    June 27, 2025
  • Mradi wa TACTIC kuimarisha Huduma za Usafirishaji kwa Miji 12 Tanzania.

    June 26, 2025
  • Halmashauri ya Mji wa Korogwe yaadhimisha Siku ya Wajane Duniani.

    June 23, 2025
  • Shule ya Msingi Kwamngumi yalima Hekari mbili za Mahindi

    June 19, 2025
  • Angalia Zote

Video

Video Zaidi

Kurasa Muhimu

  • Ukodishaji wa Ukumbi
  • Ukasanyaji wa Taka

Tovuti Zinazohusiana

  • TOVUTI YA SERIKALI
  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • MKOA TANGA
  • TUME YA AJIRA
  • PPRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Korogwe Tanga Tanzania

    S.L.P: 615 Korogwe

    Simu: 0272650050

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@korogwetc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright©2018 Korogwe Town Council. All rights reserved.