• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Mji wa Korogwe
Halmashauri ya Mji wa Korogwe

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Korogwe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Afya
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi waJamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Mazingira na Udhibiti Taka Ngumu
    • Vitengo
      • Tehama na Uhusiano
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
    • Mifugo
    • Kilimo
  • Huduma Zetu
    • Za afya
    • Kielimu
    • Za Maji
    • Za kilimo
    • Mifugo
    • Huduma za watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Elimu, afya,uchumi na maji
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Picha za Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

Korogwe Girls 1996 Group yachangia mifuko mia moja ya saruji ujenzi wa ukuta shule ya sekondari ya wasichana korogwe

Posted on: October 14th, 2019

Korogwe Girls 1996 Group  yachangia mifuko mia moja ya saruji ujenzi wa ukuta shule ya sekondari ya wasichana korogwe

Kikundi chenye wanafunzi thelathini waliomaliza shule ya sekondari ya wasichana korogwe mwaka 1996 wametoa ahadi ya kuchangia mifuko mia moja ya saruji kwa ajili ya ujenzi wa ukuta katika shule ya sekondari ya wasichana Korogwe. Ahadi hii imetolewa Oktoba 13, mwaka huu katika ukumbi wa mikutano uliopo shuleni hapo.

 Ndugu Janine Mallya  ambaye ni Mwenyekiti wa kikundi cha Korogwe Girls 1996 Group alitoa ahadi hii walipotembelea shuleni hapo  kwa lengo la kumuenzi  kwa vitendo Baba wa Taifa Mwl.J.K.Nyerere  akiwa anatimiza miaka 20 tokea atutoke duniani. Sambamba na kumuenzi baba wa taifa pia wamekuja kusisitiza umuhimu wa elimu kwa mtoto wa kike na wanawake kwa ujumla. Pamoja na kutoa ahadi ya saruji pia walikabidhi taulo za kike kwa ajili ya wanafunzi ikiwa ni ishara ya kuonyesha upendo na uzalendo kwa shule yao waliyosoma.

Nae Mwl. Mercy Kitali  akimuwakilisha Mkuu wa shule alishukuru kwa ahadi ya kutolewa  mifuko mia moja ya saruji kwa ajili ya ujenzi wa ukuta pamoja na kupokea taulo za kike kwa ajili ya wanafunzi. Alisema ni jambo la faraja sana kwa ujio wa ugeni huu, ujio wao umetoa hamasa kubwa kwa watoto wa kike waliopo  hapa shuleni kusoma kwa bidii ili kufikia malengo yao ya kuelimu na maisha kwa ujumla. Pia amefurahi kuona wanafunzi aliowafundisha kushika nyadhifa mbalimbali serikalini, makampuni binafsi na wengine kuwa wajasiriamali wakubwa hapa nchini.

Kwa upande mwingine Bi. Anjela Nyaki  ambaye ni mwanakikundi cha Korogwe Girls 1996 Group na kwa sasa ni mhifadhi mkuu wa Hifadhi ya Taifa ya Mlima Kilimanjaro aliwasisitizia wanafunzi ili kufikia malengo yao kielimu  na kimaisha kwa ujumla ni muhimu kuwa na nidhamu, kufanya ibada kila wakati pamoja na kusoma kwa bidii. Nae Mwanafunzi  Jackline Amosi amefurahi kuona wanafunzi walisoma katika shule yao wamefanikiwa kuwa wataalamu wa fani mbalimbali na wao watasoma kwa bidii  ili kupata mafanikio kama yao.

Wakati wa kuagana Bi. Anna Shanalingiwa ambaye ni katibu wa kikundi cha Korogwe Grils 1996 Group alifafanua  kuwa ujiwa wao hapo shuleni ni mwanzo naitakua muendelezo kwa siku nyingine hata hivyo amefungua milango kwa mwanafunzi yoyote aliyemaliza shule ya sekondari ya wasichana korogwe na anauzalendo wa  shule yake anaweza kuwatafuta kwa ajili ya kuchangia fedha au ushauri  kwa ajili ya maendeleo ya shule hii kupitia nambari +255758172939.

 

Matangazo

  • Tangazo la Kazi - Afya December 06, 2024
  • TANGAZO LA KAZI - AFYA November 26, 2024
  • ERMS OF REFERENCE FOR THE PROVISION OF CONSTRUCTION SUPERVISION CONSULTANCY SERVICES FOR URBAN INFRASTRUCTURE DEVELOPMENT IN KOROGWE TOWN UNDER THE TACTIC PROJECT March 09, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • Waratibu Elimu kata na Wali Wakuu wa Shule za Msingi za Mji wa Korogwe wajengewa uwezo wa usimamizi wa ufundishaji na Ujifunzaji.

    June 27, 2025
  • Mradi wa TACTIC kuimarisha Huduma za Usafirishaji kwa Miji 12 Tanzania.

    June 26, 2025
  • Halmashauri ya Mji wa Korogwe yaadhimisha Siku ya Wajane Duniani.

    June 23, 2025
  • Shule ya Msingi Kwamngumi yalima Hekari mbili za Mahindi

    June 19, 2025
  • Angalia Zote

Video

Video Zaidi

Kurasa Muhimu

  • Ukodishaji wa Ukumbi
  • Ukasanyaji wa Taka

Tovuti Zinazohusiana

  • TOVUTI YA SERIKALI
  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • MKOA TANGA
  • TUME YA AJIRA
  • PPRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Korogwe Tanga Tanzania

    S.L.P: 615 Korogwe

    Simu: 0272650050

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@korogwetc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright©2018 Korogwe Town Council. All rights reserved.