• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Mji wa Korogwe
Halmashauri ya Mji wa Korogwe

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Korogwe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Afya
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi waJamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Mazingira na Udhibiti Taka Ngumu
    • Vitengo
      • Tehama na Uhusiano
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
    • Mifugo
    • Kilimo
  • Huduma Zetu
    • Za afya
    • Kielimu
    • Za Maji
    • Za kilimo
    • Mifugo
    • Huduma za watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Elimu, afya,uchumi na maji
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Picha za Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

Ujenzi wa kituo cha afya Majengo wakamilika kwa asilimia 90

Posted on: March 13th, 2019

Ujenzi wa kituo cha afya Majengo umekamilika kwa asilimia 90 tangu ujenzi ulipoanza mwaka jana, na hivyo asilimia 10 tu za ujenzi huu zinatarajiwa kukamilika ifikapofika mwezi wa nne mwaka huu.

Kaimu mganga mkuu wa kituo cha afya Majengo Bw. Salim Bori amesema ‘ ukarabati na utanuzi wa kituo hiki umekamilika kwa asilimia 90 ambapo asilimia 10 zilizobaki ni za uwekaji wa umeme na maji tu” aliongeza kuwa miundombinu yote ya umeme na maji iko tayari kilichobaki ni upitishaji wa umeme huo pamoja na maji.

Salim Bori amesema kuwa majengo yote matano ambayo ni wodi ya wazazi, jengo la X-ray (Mionzi), jengo la upasuaji, jengo la maabara pamoja na nyumba ya mtumishi yamekamilika na hivyo yanaweza kutumika muda wowote kuanzia sasa mara baada ya kukamilisha uwekaji wa umeme na maji.

Pia amesema kuwa changamoto ilikuwa ufinyu wa eneo lakini mara baada ya kukamilika kwa majengo hayo kila kitu kitakuwa sawa na watu watapata huduma kwa urahisi tofauti na ambavyo ilivyo kwa sasa.

Aidha mhasibu wa kituo cha afya Majengo Bakari Kawambwa amesema shilingi milioni 500 ambazo walizipata mwaka jana mwezi wa tano kutoka serikalini, zimetumika vizuri na kusababisha majengo yote matano kukamilika kwa wakati bila kusuasua.

Ameongeza kuwa matarajio yao baada ya kukamilika kwa ujenzi huu, watu laki moja wataweza kuhudumiwa na hivyo huduma hii itawafikia wananchi kwa ukaribu zaidi. Amesema madaktari na wataalamu wa mionzi na maabara wapo kwaajili ya kutoa huduma bora mara baada ya kituo hicho kukamilika.

Kwa upande wa wananchi wamekuwa na muitikio mkubwa tangu kuanza kwa mradi huu wa ujenzi wa kituo cha afya hadi kufikia hatua ya mwisho na kupongeza juhudi zinazofanywa na serikali ya awamu wa tano chini ya Rais John Pombe Magufuli ili kupata huduma bora za afya.

Ujenzi wa vituo vya afya ni jambo linaloacha alama nzuri inayoonyesha utekelezaji wa kazi za serikali ili kutoa huduma bora kwa wananchi wao na kuwasogezea huduma za afya karibu na makazi yao.

Matangazo

  • Tangazo la Kazi - Afya December 06, 2024
  • TANGAZO LA KAZI - AFYA November 26, 2024
  • ERMS OF REFERENCE FOR THE PROVISION OF CONSTRUCTION SUPERVISION CONSULTANCY SERVICES FOR URBAN INFRASTRUCTURE DEVELOPMENT IN KOROGWE TOWN UNDER THE TACTIC PROJECT March 09, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • Waratibu Elimu kata na Wali Wakuu wa Shule za Msingi za Mji wa Korogwe wajengewa uwezo wa usimamizi wa ufundishaji na Ujifunzaji.

    June 27, 2025
  • Mradi wa TACTIC kuimarisha Huduma za Usafirishaji kwa Miji 12 Tanzania.

    June 26, 2025
  • Halmashauri ya Mji wa Korogwe yaadhimisha Siku ya Wajane Duniani.

    June 23, 2025
  • Shule ya Msingi Kwamngumi yalima Hekari mbili za Mahindi

    June 19, 2025
  • Angalia Zote

Video

Video Zaidi

Kurasa Muhimu

  • Ukodishaji wa Ukumbi
  • Ukasanyaji wa Taka

Tovuti Zinazohusiana

  • TOVUTI YA SERIKALI
  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • MKOA TANGA
  • TUME YA AJIRA
  • PPRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Korogwe Tanga Tanzania

    S.L.P: 615 Korogwe

    Simu: 0272650050

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@korogwetc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright©2018 Korogwe Town Council. All rights reserved.