• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Mji wa Korogwe
Halmashauri ya Mji wa Korogwe

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Korogwe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Afya
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi waJamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Mazingira na Udhibiti Taka Ngumu
    • Vitengo
      • Tehama na Uhusiano
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
    • Mifugo
    • Kilimo
  • Huduma Zetu
    • Za afya
    • Kielimu
    • Za Maji
    • Za kilimo
    • Mifugo
    • Huduma za watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Elimu, afya,uchumi na maji
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Picha za Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

Viongozi wa umma wapewa mafunzo juu ya magonjwa yasiyopewa kipaumbele

Posted on: April 3rd, 2019

Magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele ni magonjwa ambayo yamo ndani ya jamii hasa jamii masikini.Magojwa hayo ni Matende na Mabusha, Kichocho, Minyoo ya tumbo, Usubi, na Trakoma.

Mratibu wa mafunzo  kutoka Wizara ya Afya Dk. Joyceline Sambo amesema dhumuni la mafunzo hayo ni kuwafanya viongozi wanaoongoza jamii kuwa na uelewa na pia kutoa elimu juu ya madhara ya magonjwa hayo kwani hayapewi kipaumbele kama yalivyo magonjwa mengine, mafunzo hayo yametolewa kwa viongozi mbalimbali wakiwemo madiwani.

Ameongeza kuwa kwakuwa wao ni viongozi hivyo kupitia wao wataweza kuwafikia wananchi wao kwa karibu zaidi.

Dk Sambo amesema “magonjwa haya ni kama kichocho ambacho husababishwa na minyoo ya jamii ya Schistosoma ambapo binadamu hueneza vimelea vya ugonjwa huu kwa kutojisaidia kwenye choo na kupelekea kinyesi/ mkojo kuchangamana na vyanzo vya maji, lakini pia kuna ugonjwa wa matende na mabusha ambao husababishwa na minyoo aina ya Wechereria Bancrofti unaosambazwa na mbu aina zote”.

Amesema ugonjwa wa usubi ambao husababishwa na minyoo, minyoo hiyo inaenezwa na inzi weusi wadogo ambao hukaa kandokando ya mito yenye maji yaendayo kasi, magonjwa mengine ni trakoma na minyoo ya tumbo.

Dk Sambo ameiomba jamii kutunza mazingira kwani magojnwa haya husababishwa na utunzaji mbovu wa mazingira na usafi kwa ujumla.

 Kwa upande wake diwani wa kata ya Mgombezi Bw. Omary Kassim Chafesi amesema “nimefurahia mafunzo haya na kuyapokea vizuri  na kwa jinsi nilivyoelewa nitawaelimisha jamii ninayoiongoza katika mikutano yangu yote ya nje na ndani”.

Diwani Omary ameongeza kuwa magonjwa haya husumbua jamii za watu wenye hali ya chini na wao kupuuzia kwa kujua kuwa ni magonjwa ya kawaida lakini kutokana na uelewa alioupata kupitia mafunzo haya atahakikisha anatoa mafunzo kwa jamii ili waepukane na magonjwa.

Pia amesema kuwa atatoa elimu kwa  jamii juu ya usafi wa miili yao na mazingira  yanayowazunguka ili kusaidia kutunza vyanzo vya maji na kuepukana na magonjwa.

Nae diwani wa viti maalum Wilhelma Mpangala amesema “ semina nimeikubali na nimeipenda kutokana na elimu kubwa niliyoipata leo kwakuwa sikujua kwamba hata sisi wanawake tuna mabusha lakini kupitia elimu hii nimejua”.

Aidha ameongeza kuwa “nitahakikisha naelimisha jamii yangu yote  na nitahakikisha nawaambia wale watakaotoa dawa kufatilia kwa makini kama watu wamekunywa kweli”.

Nchini Tanzania wananchi wote, wapo hatarini kuambukizwa magonjwa haya. Inakadiriwa kuwa watu milioni 5 wameshaathirika na mojawapo ya magonjwa hayo.

Matangazo

  • Tangazo la Kazi - Afya December 06, 2024
  • TANGAZO LA KAZI - AFYA November 26, 2024
  • ERMS OF REFERENCE FOR THE PROVISION OF CONSTRUCTION SUPERVISION CONSULTANCY SERVICES FOR URBAN INFRASTRUCTURE DEVELOPMENT IN KOROGWE TOWN UNDER THE TACTIC PROJECT March 09, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • Waratibu Elimu kata na Wali Wakuu wa Shule za Msingi za Mji wa Korogwe wajengewa uwezo wa usimamizi wa ufundishaji na Ujifunzaji.

    June 27, 2025
  • Mradi wa TACTIC kuimarisha Huduma za Usafirishaji kwa Miji 12 Tanzania.

    June 26, 2025
  • Halmashauri ya Mji wa Korogwe yaadhimisha Siku ya Wajane Duniani.

    June 23, 2025
  • Shule ya Msingi Kwamngumi yalima Hekari mbili za Mahindi

    June 19, 2025
  • Angalia Zote

Video

Video Zaidi

Kurasa Muhimu

  • Ukodishaji wa Ukumbi
  • Ukasanyaji wa Taka

Tovuti Zinazohusiana

  • TOVUTI YA SERIKALI
  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • MKOA TANGA
  • TUME YA AJIRA
  • PPRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Korogwe Tanga Tanzania

    S.L.P: 615 Korogwe

    Simu: 0272650050

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@korogwetc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright©2018 Korogwe Town Council. All rights reserved.