• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Mji wa Korogwe
Halmashauri ya Mji wa Korogwe

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Korogwe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango Miji na Ardhi
      • Afya
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii na Ustawi waJamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Mazingira na Udhibiti Taka Ngumu
    • Vitengo
      • Tehama na Uhusiano
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Nyuki
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
    • Mifugo
    • Kilimo
  • Huduma Zetu
    • Za afya
    • Kielimu
    • Za Maji
    • Za kilimo
    • Mifugo
    • Huduma za watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Elimu, afya,uchumi na maji
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Picha za Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio

Wilaya ya Korogwe yapata mafunzo ya ufugaji wa nyuki

Posted on: March 16th, 2020

 Wilaya ya Korogwe yapata mafunzo ya ufugaji wa nyuki

Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Tanzania Mh. Edmund Mndolwa amefungua mafunzo  ya ufugaji wa nyuki  kwa Mkoa wa Tanga. Mafunzo ambayo pia yalihudhuriwa na Mh. Kissa Kasongwa ambaye ni mkuu wa Wilaya ya Korogwe pamoja na Wakurugenzi kutoka Halmashauri zote mbili za  Wilaya ya Korogwe. mafunzo hayo yalizinduliwa  Machi 16, mwaka huu katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Mji wa Korogwe.

Akizungumzia mafunzo hayo Mh. Edmund Mndolwa ambaye ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya wazazi Tanzania alisema “lengo la mafunzo haya ni kuhamasisha ufugaji nyuki kwa vijana na vikundi kwa ujumla ili wajikwamue kiuchumi”. Mh. Mndolwa  alifafanua kuwa kwa sasa ufugaji wa nyuki unalipa na ni  muda muafaka kwa vijana kujiajiri kupitia ufugaji wa nyuki

Katika hatua nyingine Mh. Mndolwa  amewahakikishia wafugaji wa nyuki kuwa  kuna soko la kutosha la bidhaa za nyuki ndani na nje ya nchi. Alitoa ushauri kwa wafugaji watumie mizinga ya kisasa ili wapate asali ya kutosha pamoja na bidhaa nyingine za nyuki. Pia alitoa maelekezo kwa Jumuiya ya wazazi katika kila Wilaya  watenge hekari moja kwa ajili ya ufugaji wa nyuki.

Nae Bi. Groria Joseph mwezeshaji wa mafuzo  kutoka chuo cha International Beekiping Openi School kilichopo  Mkoani  Singida alisema “ ni vyema vijana tukachangamkia fursa ya ufugaji wa nyuki  ili kuongeza kipato pamoja na kupata lishe bora kwa ajili ya afya zetu” Bi. Groria alifafanua kuwa ufugaji wa nyuki una tija kubwa kwa mfugaji  ikiwepo kupata  bidhaa  kama vile asali, nta, pamoja na gundi ya nyuki. Bidhaa nyingine ni  sumu ya nyuki, supu ya nyuki,  maziwa ya nyuki na chavua.

 Kwa upande mwingine Bi. Rehema Kazenga ambaye ni mshiriki wa mafunzo ya ufugaji wa nyuki kutoka Mji wa Korogwe aliishukuru Jumuia ya Wazazi Tanzania kwa kuandaa mafunzo ya ufugaji wa nyuki kwa kuwa mafunzo  haya yatawasaidia vijana pamoja na vikundi vyengine kujiajiri kupitia ufugaji wa nyuki.

Matangazo

  • Tangazo la Kazi - Afya December 06, 2024
  • TANGAZO LA KAZI - AFYA November 26, 2024
  • ERMS OF REFERENCE FOR THE PROVISION OF CONSTRUCTION SUPERVISION CONSULTANCY SERVICES FOR URBAN INFRASTRUCTURE DEVELOPMENT IN KOROGWE TOWN UNDER THE TACTIC PROJECT March 09, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • Waratibu Elimu kata na Wali Wakuu wa Shule za Msingi za Mji wa Korogwe wajengewa uwezo wa usimamizi wa ufundishaji na Ujifunzaji.

    June 27, 2025
  • Mradi wa TACTIC kuimarisha Huduma za Usafirishaji kwa Miji 12 Tanzania.

    June 26, 2025
  • Halmashauri ya Mji wa Korogwe yaadhimisha Siku ya Wajane Duniani.

    June 23, 2025
  • Shule ya Msingi Kwamngumi yalima Hekari mbili za Mahindi

    June 19, 2025
  • Angalia Zote

Video

Video Zaidi

Kurasa Muhimu

  • Ukodishaji wa Ukumbi
  • Ukasanyaji wa Taka

Tovuti Zinazohusiana

  • TOVUTI YA SERIKALI
  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • MKOA TANGA
  • TUME YA AJIRA
  • PPRA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Korogwe Tanga Tanzania

    S.L.P: 615 Korogwe

    Simu: 0272650050

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: info@korogwetc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright©2018 Korogwe Town Council. All rights reserved.